Sep 14, 2016

Wafanyakazi wa Sekta Hii Serikalini Ndio Wanao Ongoza Kwa Mishahara Mikubwa


SERIKALI imesema wafanyakazi wa sekta ya afya ndio wanaopokea viwango vikubwa vya mishahara wakifuatiwa na wale wa sekta ya elimu nchini.

Taarifa hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Angela Kairuki, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Zubeda Sakuru (Chadema).

Katika swali lake, Sakuru alitaka kujua Serikali inakabiliana vipi na changamoto za masilahi kwa watumishi katika sekta ya afya.

Sakuru alisema kuna matukio ya vifo visivyo vya lazima vinavyotokana na ukosefu wa motisha kwa madaktari na wauguzi, ambao wanalipwa viwango vidogo vya mishahara na hawalipwi posho zao kwa wakati.

Akijibu swali hilo, Kairuki alisema Serikali imeendelea na jitihada za kuboresha mishahara ya watumishi wake, ikiwamo wataalamu wa sekta ya afya kwa kuzingatia uwezo wa kifedha.

Alisema kwamba mishahara huzingatia ngazi ya elimu, ambapo ngazi ya astashahada kwa upande wa Serikali Kuu ni Sh 390,000, kada ya walimu Sh 419,000, wauguzi Sh 432,000 na madaktari ni Sh 432,000.

Kwa upande wa stashahada, Serikali Kuu ni Sh 525,000, walimu 530,000 wauguzi 680,000 na madaktari ni Sh 680,000.

Kairuki alisema ngazi ya shahada kwa upande wa Serikali Kuu ni Sh 710,000, walimu 716,000, wauguzi 980,000 na madaktari ni Sh 1,480,000.

Pamoja na hayo, alisema Serikali inaendelea na utafiti wa tathmini ya kazi na itakapokamilika, itapanga upya mishahara na motisha kwa watumishi wote wa umma ikiwamo sekta hiyo.

“Kati ya mwaka 2010/11 hadi mwaka 2016/17, vianzia vya mishahara kwa kada za wauguzi vimeongezeka kutoka shilingi 614,000 hadi 980,000 kwa mwezi kwa wahitimu wa shahada.

“Vimeongezeka pia kutoka shilingi 425,000 hadi shilingi 680,000 kwa wahitimu wa stashahada na shilingi 260,000 hadi shilingi 432,000 kwa wahitimu wa astashahada.

“Kwa kada ya madaktari na maofisa tabibu katika kipindi hicho, vimeongezeka kutoka shilingi 886,800 hadi shilingi 1,480,000 kwa wahitimu wa shahada na shilingi 425,000 hadi shilingi 680,000 kwa wahitimu wa stashahada na shilingi 260,000 hadi shilingi 432,000 kwa wahitimu wa astashahada.

“Pamoja na hayo, Serikali itaendelea kuboresha masilahi ya waatumishi kadiri uwezo wake wa kulipa utakavyoimarika,” alisema Kairuki.

Wakati huo huo, Serikali imewaagiza waajiri wote nchini kuhakikisha wanatenga fedha za uhamisho na za marekebisho ya mishahara kabla ya hatua yoyote kufanyika.

Agizo hilo lilitolewa bungeni jana na Waziri Kairuki wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima (CCM), aliyetaka kujua Serikali ina mpango gani wa kupandisha mishahara ya watumishi wa umma kwa kuwa kila mwaka inapofika Julai, hupandisha vyeo na mishahara kwa watumishi wa umma.

Awali katika swali la msingi, mbunge huyo aliuliza Serikali ina mpango gani wa kuyalipa madeni ya watumishi wa umma, vilevile alihoji mkakati wake wa kuhakikisha haina madeni tena.

Katika majibu hayo, Kairuki hakulitolea ufafanuzi swali la nyongeza, badala yake alijielekeza katika kujibu madeni ya watumishi wa umma.

Alisema ni kweli kulikuwa na malimbikizo, lakini tangu kuanzishwa kwa mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara, malimbikizo yamepungua.

Kairuki alisema ili kukabilina na changamoto ya malimbikizo ya madeni, ni vema waajiri wazingatie sheria na kanuni kwa kuhakikisha wanalipa fedha kwa wakati, zikiwamo za matibabu na posho, ambazo zimekuwa zikilalamikiwa.

“Serikali inatoa wito kwamba mtumishi yeyote asihamishwe kama hakuna fedha za uhamisho, pia na za marekebisho ya mishahara. Mambo haya yafanywe pale fedha zinapokuwapo,” alisema Kairuki

Sambamba na hilo, waziri huyo alieleza kwamba nafasi za kukaimu lazima zitolewe taarifa ili mtumishi anayekaimu nafasi husika aweze kulipwa stahiki yake kwa wakati.

Akizungumzia mpango wa Serikali wa kukabiliana na mlundikano wa madeni ya watumishi, Kairuki alieleza kuwa inaendelea kupokea na kuhakiki madai ya watumishi wa umma yanayohusu mishahara na kuyalipa kwa kadiri ya uwezo wake wa kifedha.

“Katika mwaka wa fedha 2014/2015 Serikali ililipa madai ya malimbikizo ya mshahara ya shilingi 55,293,372,627.37 ambayo yalilipwa kwa watumishi 55,688 waliokuwa na madai yaliyotokana na kupandishwa vyeo, ajira mpya na sababu nyinginezo.

“Kwa mwaka wa fedha 2015/2016 Serikali imeendelea kulipa madai ya malimbikizo ya mshahara ya watumishi wa umma ambapo hadi kufikia Juni 2016 watumishi 31,032 walilipwa jumla ya Sh 28,929,095,373.89,” alisema Kairuki

Aliongeza kuwa madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi 7,871 yenye zaidi ya Sh bilioni 13.7 yamehakikiwa na kuingizwa kwenye mfumo wa taarifa za kiutumishi na mishahara na sasa yanasubiri kulipwa.

Kairuki alisema madai ya watumishi 8,776 yenye zaidi ya Sh bilioni 15.5 yanaendelea kuhakikiwa ili yaingizwe kwenye mfumo kwa ajili ya kufanya malipo.

Waziri huyo alieleza kuwa katika shughuli za kila siku madeni huzalishwa, hivyo azma ya Serikali ni kuhakikisha yanalipwa mara yanapojitokeza.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger