Sep 3, 2016

Wanaoficha Fedha ni Wahujumu Uchumi

KUTOKANA na kauli ya Rais John Magufuli aliyoitoa juzi jijini Dar es Salaam kuwa anafahamu wapo wananchi wameficha fedha nyumbani, wachumi wametoa maoni yao na kusema hao ni wahujumu uchumi na wanapaswa kutafutwa na vyombo vya dola na washtakiwe.

Akitoa maoni yake jana jijini Dar Salaam, Mhadhiri Mwandamizi wa Masuala ya Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana alisema uhai wa uchumi ni uwepo wa mzunguko wa fedha za kutosha.

Dk Bana alisema uchumi wa taifa lolote ni lazima katika kazi na shughuli za kimaendeleo na kijamii fedha ziwepo ili kufanya mzunguko uongezeke na kukuza uchumi, lakini uchumi huathirika iwapo kutatokea watu wanauhujumu kwa njia mbalimbali.

“Baadhi ya watu wanaamua kuficha fedha na hiyo inaathiri mtiririko wa fedha na wanaleta mfumuko wa bei, hawa sasa wanafanya hila kuzorotesha uchumi,” alisema Dk Bana na kuongeza kuwa kama fedha ni halali, kwa nini mtu afiche na kusema kuwa benki ndio mahali pekee salama kwa kutunza fedha na kama wapo watu wanatoa fedha benki na kuzificha majumbani wana hila za kuhujumu uchumi.

Alifafanua kuwa katika uhai wa taifa lolote kukiwa na mzunguko wa fedha wa kutosha katika jamii, husaidia kuimarisha thamani ya fedha na kwamba kama mzunguko huo utaathiriwa kwa makusudi unaweza sababisha hali mbaya ya uchumi.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa jambo la msingi la kufanya sio kuchapisha fedha mpya, bali ni kuhakikisha serikali inawabana wala rushwa na mafisadi ambao ndio wanachangia uchumi kuyumba.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania, Johnson Minja alisema wanaoficha fedha kwa makusudi ni wahujumu uchumi na wanapaswa kusakwa na kuchukuliwa hatua.

Minja alisema fedha sio mali ya mtu binafsi ni mali ya serikali na inapaswa kutumika kwa makusudi stahiki ambayo ni pamoja na kumwezesha mwananchi kufanya malipo mbalimbali na ndio maana fedha zote zina namba na saini ya waziri husika pamoja na gavana wa Benki Kuu.

“Watu waelewe kuwa fedha sio mali yao hata kama unazimiliki ni mali ya serikali na hupaswi kuzificha, ni lazima ziingie kwenye mzunguko wa fedha unapoficha ni kosa la kuhujumu uchumi na unapaswa kuchukuliwa hatua,” alisema Minja.

Alisema watu wanaoficha fedha nyumbani wengi wao ni wahalifu na wanafanya hivyo kwa sababu wanafahamu fedha hizo wamezipata isivyo halali na ni vyema vyombo vya uchunguzi nchini vikawamulika na kuwashughulikia kwa sababu wanahujumu uchumi kwa maslahi binafsi.

Hata hivyo, alisema pamoja ya kuwepo na tatizo hilo la baadhi ya watu kuficha fedha kwa makusudi, wapo pia wananchi walioficha fedha zao kwa sababu ya uelewa mdogo wa masuala ya fedha.

Alisema hivi sasa nchini kuna tatizo la kusuasua kwa mzunguko wa fedha unaosababishwa na kupanda kwa bei za kodi mbalimbali hivyo wananchi wana hofu ya kuagiza bidhaa nje kwa kuwa watashindwa kuuza kutokana na bei kuwa kubwa.

Alishauri serikali kuangalia jinsi ya kurudisha uchumi katika hali ya kawaida ili biashara zifanyike na watu waagize bidhaa nje

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger