Oct 6, 2016

UCHAMBUZI: Hongera Rais Magufuli Kwa Kukwepa Mtego huu

Katika mambo ambayo najiuliza lakini sipati majibu yake, ni hatua ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, kupendekeza ndege zetu mbili mpya ziitwe ‘Hapa Kazi Tu’.

Kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’, ilitumiwa na Rais John Magufuli katika kipindi cha kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2015, wakati huo Magufuli akipeperusha bendera ya CCM nafasi ya urais.

Katika uzinduzi wa ndege hizo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jullius Nyerere (JNIA), Profesa Mbarawa alimuomba Rais Magufuli, aridhie ndege hizo zipewa jina la ‘Hapa Kazi Tu’.

Profesa huyo ambaye binafsi naweza kusema alikuwa anajipendekeza kwa Rais, alienda mbali na kudai uamuzi wa kuzipa ndege hizo jina hilo ni mapendekezo ya pamoja na wenzake wizarani.

Nilipomsikiliza Waziri huyo akitoa pendekezo hili la kuipa jina la ‘kisiasa’, ndege itakayotumiwa na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kujiendesha kibiashara, nilishtuka. Sikuamini nilichosikia.

Kabla sijaeleza kwa nini sikubaliani na pendekezo hilo la Profesa Mbarawa, lazima nichukue fursa hii kumpongeza Rais Magufuli kwamba katika hotuba yake yote ya dakika 50 hakugusia pendekezo hilo.

Rais alisema: “Hii ndege haikuandikwa CCM kwa hiyo meya hapa ataipanda, Mbowe (Freeman) ataipanda, CCM wataipanda, Lipumba (Ibrahim) ataipanda na asiye na chama ataipanda”.

“Ni ndege za Watanzania na ni lazima tujifunze sisi Watanzania kujivunia utanzania wetu.” Alisisitiza Rais Magufuli, kauli ambayo ilionekana kujibu ombi la Profesa Mbarawa japo siyo moja kwa moja.

Ndege hizi ni za Watanzania na zimenunuliwa kwa fedha za Watanzania wote pasipo kuingiza itikadi za kisiasa. Namshukuru na kumpongeza Rais wangu kwa kutoingia katika mtego huu wa Profesa Mbarawa.

Nilijiuliza maswali mengi, hivi kama Rais mstaafu Jakaya Kikwete, angekuwa amefanikiwa kununua ndege katika kipindi chake nazo zingepewa jina la ‘Ari mpya, Kasi mpya na Nguvu mpya’?

Hakuna tafsiri nyingine yoyote inayoweza kueleweka kwa nini Profesa Mbarawa aliamua kupendekeza jina hilo wakati akijua ndege hizi zinajiendesha kibiashara.

Bahati nzuri katika kipindi kifupi nilichomfahamu Rais Magufuli anatanguliza utaifa na uzalendo kwanza na mambo ya vyama ni baadaye na hili amelithibitisha mara zote kwenye hotuba zake.

Kwanini napinga jina la ‘Hapa Kazi Tu’? Ni dhana rahisi kwamba katika biashara ya usafiri wa anga ni lazima tuje na mkakati wa kuitangaza nchi na vivutio vyake, siyo itikadi za vyama.

Tukitoa mfano, mdogo wa bidhaa. Huwezi amini kila mtalii aliyekuja kupanda Mlima Kilimanjaro au kutembelea mbuga za wanyama na kupewa orodha ya bidhaa atachagua zilizo na majina ya Kilimanjaro, Mikumi  au Serengeti.

Ni kwa sababu ni vivutio maarufu duniani ambavyo vinatangazwa kimataifa, hivyo mtalii anapotumia bidhaa hizo anabaki na kumbukumbu ya hifadhi na vivutio alivyoviona Tanzania.

Mara zote tunalalamika kuwa majirani zetu Kenya wanatangaza kimataifa kuwa Mlima Kilimanjaro uko Kenya na hii imewafanya watalii wengi kushukia nchini humo badala ya Tanzania ulipo.

Sasa leo badala ya kutumia fursa za uwapo wa ndege za ATCL ambazo baadaye zitafanya safari za kimataifa, kutangaza vivutio vyetu tunataka kutangaza ‘Hapa Kazi Tu’ ili tufanikiwe nini?.

Binafsi naamini Menejimenti ya ATCL italifanyia kazi suala hilo na kuja na jina ambalo litasaidia kuitangaza Tanzania kimataifa.

By Daniel Mjema
0769600900



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger