Oct 6, 2016

CHADEMA Wazua Balaa Umeya wa Kinondoni

Wakati mchakato wa uchaguzi wa meya na naibu wake ukiendelea, suala la idadi ya madiwani wa viti maalumu wa Chadema katika Manispaa ya Kinondoni limeibua mvutano mpya kati ya chama hicho na ofisi ya mkurugenzi mtendaji.

Mvutano huo umejitokeza baada ya Mkurugenzi wa Kinondoni, Aron Kagurumjuli kutoa barua inayoeleza kuwa kutakuwa na madiwani viti maalumu wanawake wasiopungua theluthi moja ya madiwani wa kuchaguliwa wa Chadema.

Kwa mantiki hiyo, Chadema ambayo ina madiwani wa kuchaguliwa saba itakuwa na madiwani watatu wa viti maalumu. Kwa hiyo majina yasiyopungua matatu ndiyo yatakayowasilishwa kuunda baraza jipya la madiwani.

Hata hivyo, Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo alipinga maelezo hayo ya mkurugenzi akisema: “Tayari nimeshamwandikia barua mkurugenzi kumweleza. Tungekuwa tunatoka katika uchaguzi mkuu ningekubaliana na hoja ya Kagurumjuli, lakini kwa hali ilivyo sasa siwezi kukubaliana naye kwa sababu baraza likiitishwa madiwani hawatakula kiapo kama awali.”

Kuhusu madai hayo Kagurumjuli alisema: “Nasimamia sheria, sifuati matakwa ya mtu. Nadhani wao wanapingana na sheria. Sielewi presha inatoka wapi. Wa kushinda atashinda na wa kukosa atakosa kulingana na idadi ya wajumbe wake na hakuna atakayeonewa.”

Alisisitiza kuwa kulingana na sheria hiyo na idadi ya madiwani wa kuchaguliwa wa Chadema, chama hicho hakiruhusiwi kuongeza diwani mwingine. Kagurumjuli hakuwa tayari kutaja idadi ya wajumbe watakaounda baraza la madiwani na kusema kwamba anasubiri majina ya madiwani kutoka CUF, Chadema na CCM.

Lakini Kilewo alisema msimamo wa Chadema uko palepale wa kuhakikisha madiwani wanne wanabaki Kinondoni na kwamba hakuna mwenye mamlaka ya kuengua mjumbe isipokuwa kifo na mahakama.

“Ubungo hakuna tatizo. Ingawa maelezo yanafanana ya wajumbe watatu kutakiwa kulingana na idadi ya madiwani wa kuchaguliwa. Ishu ipo Kinondoni kwa sababu madiwani wetu wa viti maalumu wengi walikubaliwa,” alisema Kilewo.

Kuhusu umeya baada ya manispaa hizo kugawanywa, Kilewo alisema jina la Mustafa Muro, Diwani wa Kinondoni, ndilo lililopendekezwa na kupelekwa kwa ajili ya kugombea umeya wa Kinondoni huku Boniface Jacob akiteuliwa kugombea Ubungo.

Wakati Kilewo akisema hayo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge alisema mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi ya umeya na naibu meya katika manispaa hizo ulitarajiwa kukamilika jana jioni.

“Mchakato huu ulianza muda mrefu lakini leo (jana), jioni ndiyo kilele chake. Wagombea watakaopatikana ni mahiri na CCM ipo fiti tunasubiri mechi uwanjani,” alisema Madenge.

Kwa nyakati tofauti, Manispaa za Kinondoni na Temeke zilifanya mgawanyo wa madiwani baada ya Serikali kuzigawanya na kuunda halmashauri za Ubungo na Kigamboni.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger