Oct 9, 2016

Mvutano wa Siasa Zanzibar...CUF Yatoa Masharti Mawili Kwa Serikali

Akizungumza na Mwandishi wa Habari hii katika mahojiano maalumu mjini Zanzibar juzi, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CUF, Ismail Jussa Ladhu, alisema masharti hayo mawili yanayopaswa kuzingatiwa ni kuhakikisha kuwa panaundwa Serikali ya Mseto na jambo la pili, ni sharti kwa serikali hiyo kuandaa uchaguzi mwingine visiwani humo utakaotoa fursa ya wananchi kujichagulia kwa uhuru viongozi wanaowataka.

Aliyekuwa mgombea wa CUF katika uchaguzi mkuu uliopita, Maalim Seif Shariff Hamad, aliwaambia waandishi wa habari siku chache baada ya uchaguzi wa awali uliofanyika Oktoba 25, 2015 kuwa anaelekea kushinda kwa zaidi ya asilimia 50 na kuitaka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutenda haki. Hata hivyo, ilipofika Oktoba 28, 2015, Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha, alitangaza kufutwa kwa uchaguzi huo kutokana na kile alichoeleza kuwa ni kuwapo kwa kasoro nyingi.

Uamuzi huo wa Jecha ulipingwa na CUF na pia waangalizi mbalimbali wa ndani na wa kimataifa. Katika uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, 2016, CUF iligoma kushiriki na kuitaka ZEC iendelee na majumuisho ya kura zilizotokana na uchaguzi wa Oktoba 25. Matokeo ya uchaguzi wa marudio yakaonyesha kuwa mgombea wa CCM, Rais Shein, ameshinda kwa zaidi ya asilimia 90 ya kura halali zilizopigwa.

Alipoulizwa kuhusu uwezekano wa CCM na CUF kurudi mezani na kufanya mazungumzo kwa nia ya kuona kuwa Zanzibar haiwi na mvutano wa kisiasa unaoelekea kuwagawa watu kiitikadi, Jussa alisema hilo ni jambo zuri na wao siku zote wamekuwa wakisisitiza umuhimu wa siasa za mazungumzo na siyo za kuegemea matumizi ya “nguvu na mabavu”.

“CUF siku zote imekuwa mstari wa mbele. Haijawahi kukataa mazungumzo hata siku moja kwa sababu tunaamini kuwa siasa inafanywa kwa mazungumzo, siyo kwa kutumia mabavu na vitisho, hayo yamepitwa na wakati katika dunia ya leo,” alisema Jussa na kuongeza:

“Na niseme kwamba pamoja na kuamini kuwa tumeshinda kihalali katika uchaguzi wa Oktoba mwaka jana, bado CUF imenyoosha mkono na kutoa mapendekezo kupitia kiongozi wetu Maalim Seif Sharif Hamad, hasa akiwa katika ziara nchi za nje, kutaka pafanyike mazungumzo yatakayowezesha kuundwa kwa Serikali ya Mpito na baadaye kukubaliana juu ya kufanyika kwa uchaguzi mwingine.”

Akieleza zaidi, Jussa alisema wapo wananchi ambao hadi sasa wangali na kinyongo kutokana na kukasirishwa na hila zilizofanyika katika uchaguzi mkuu uliopita.

“Siyo kama watu hawazikani, wapo wananchi wamekasirishwa mno na kitendo kilichofanyika kwa sababu hawakutarajia Zanzibar kurejeshwa ilipotoka…hawaipi ushirikiano Serikali. Bila shaka pana haja ya mazungumzo lakini ili mazungumzo hayo yafanyike panahitajika kwanza kutambua tatizo kwa pande zote mbili zinazohasimiana. Pili kuwe na utashi wa kuona kuwa mazungumzo hayo yanaleta tija.

 “Na ndio maana sisi CUF tunasema kwamba mazungumzo kati ya CCM na CUF tumeshafanya mengi lakini hayaonekani kwamba yanachukuliwa kwa umakini, kuna haja ya kuwa na mpatanishi ambaye atasimamia mazungumzo hayo na awe mtu anayeheshimika na mwenye uadilifu, atoke nje ya Tanzania au nje ya Afrika.”

Aidha, Jussa alisema Zanzibar ni ya wananchi wote wa Zanzibar bila kujali itikadi za vyama na hivyo, kuendelea kuvutana hakuwanufaishi wananchi.

“Kwa upande wa Bara wanapaswa kutambua kuwa hali inayoendelea sasa haina maslahi hata katika Muungano…muungano hauwezi kujengwa kwa kuidhoofisha Zanzibar. Tunapaswa tushirikiane ili Zanzibar iwe imara, yenye umoja na mshikamano,” alisema Jussa

 – Nipashe

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger