Oct 26, 2016

UJAMBAZI Wakutisha Dar, Yafunga Mtaa Kwa Saa Mbili, Yapora Mamilioni

NI ujambazi wa kutisha. Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na kuibuka na wizi unaofanywa na majambazi katika maeneo mbalimbali nchini.

Hatua hiyo inatokana na majambazi hao kuibuka na mbinu mpya kila kukicha katika matukio mbalimbali ambayo sasa yamekuwa yakishika kasi.

Mbali na mbinu ya kutumia pikipiki, majambazi hayo pia huvamia vibanda vya kutoa huduma za fedha, kuiba magari na hata wakati mwingine kuua.

Katika hali iliyovuta hisia za watu wengi, juzi usiku majambazi yalifunga mtaa kwa saa mbili na kupora fedha kwa watoa huduma ya fedha kwa njia ya simu katika eneo la Tabata jijini Dar es Salaam.

Mbali na maduka, watu wengine waliokuwa nje nao pia waliporwa simu na fedha. Hata hivyo thamani ya fedha na vitu vilivyoporwa havikujulikana mara moja.

Tukio hilo lililoshtua wakazi wengi wa mitaa ya Kimanga na Kisukuru wilayani Ilala, Dar es Salaam, ni la pili kutokea ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.

Awali mwezi uliopita, majambazi wenye silaha walimuua kwa risasi askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na baadaye kumpora fedha Sh milioni tano, nje ya geti la nyumbani kwake Mtaa wa Kimanga, saa tano asubuhi.

Tukio la juzi lilitokea katika moja ya maduka yaliyoko pembezoni mwa kituo cha daladala cha Jiandae kilichopo Tabata Kimanga, ambako majambazi wanaokadiriwa kuwa zaidi ya wanne yaliingia dukani na kuwaamuru wafanyakazi kutoa fedha zote za mauzo ya siku, huku wakiwatishia kwa mapanga na bastola.

Mmoja wa wafanyakazi wa kike katika maduka hayo alipoteza fahamu baada ya tukio hilo na alikimbizwa hospitali kwa matibabu.

Licha ya idadi kubwa ya watu katika eneo hilo lenye biashara mbalimbali wakati wa jioni, majambazi hao hawakujali, walifanya uporaji huo na baadaye kutokomea kwa kutumia pikipiki aina ya Boxer.

Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia MTANZANIA jana kuwa kwa muda wa dakika tano hakuna gari iliyoruhusiwa kwenda au kutoka Kimanga.

“Majambazi waliwaamuru wenye  magari kutokukatiza eneo hilo, huku waenda kwa miguu wakiamriwa kuondoka haraka.

“Katika hali ya kawaida ni vigumu kuamini kama majambazi wanaweza kuvamia na kupora vitu katika maduka matatu kwa mpigo halafu wakatoweka bila kukamatwa,” alisema shuhuda huyo aliyekataa kutajwa jina.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kimanga, Manase Mjema, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alisema majambazi hao yalikuwa yamejiandaa na yalitumia silaha kubwa.

“Awali kabla ya kufyatua risasi yaliwaamuru wafanyakazi wa maduka yanayofanya biashara kupitia miamala ya simu kutoa fedha zote za mauzo, vijana walikuwa ngangari kidogo, hivyo majambazi waliamua kupiga risasi tatu hewani ndipo waliamua kutoa fedha walizokuwa nazo,” alisema.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo alikiri kuwapo kwa ulinzi hafifu katika mtaa wake, huku pia akishauri Jeshi la Polisi kuimarisha doria mitaani kwa kuongeza askari wasiokuwa na sare ili wasitambulike kwa urahisi.

“Nikiri kwamba ulinzi wetu wa mtaa wakati wa usiku bado ni mdogo, tunaomba polisi nao waangalie mbinu mbadala za kukabiliana na uhalifu, na hasa ujambazi huu wa kutumia silaha za moto. Eneo la Tabata hivi sasa limekumbwa na matukio mengi ya ujambazi, kwa hiyo lazima mbinu nazo zibadilike,” alisema Mjema ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kimanga (Chadema).

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya, alikiri kupokea taarifa za ujambazi na tayari askari wake wameanza uchunguzi ili kuwabaini wahalifu hao.

“Nitoe ombi na nisisitize wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kutokomeza vitendo vyote vya uhalifu. Viongozi wote wa mitaa watupatie taarifa za watu wanaowatilia shaka, nasi tutazifanyia kazi,” alisema Kamanda Mkondya.

Katika siku za hivi karibu kumeibuka matukio ya ujambazi katika maeneo mbalimbali nchini huku wakiibua mbinu mpya za kufanikisha wizi huo.

Kutokana na hali hiyo majambazi hao wamekuwa wakitumia pikipiki kwa ajili ya kutekeleza uvamizi kwenye matukio hayo na hata wakati mwingine kuua watu na kujeruhi.

Katika mfululizo wa matukio ya ujambazi jijini Dar es Salaam, Agosti 23, mwaka huu, askari wanne wa Jeshi la Polisi waliuawa baada ya majambazi kuvamia Tawi la Benki ya CRDB lililopo Mbande, wilayani Temeke.
Majambazi hao wanaokadiriwa kufikia 14, wakati askari hao wakibadilishana lindo, waliibuka ghafla na kuanza kurusha risasi na askari mmoja aliyekuwa lindo alifanikiwa kukimbia.

Kutokana na foleni katika barabara nyingi za Dar es Salaam pamoja na miundombinu ya makazi yasiyokuwa rasmi, matukio mengi ya ujambazi yanayoripotiwa ni ya kutumia pikipiki, hivyo kuwapa wakati mgumu polisi ambao mara nyingi wanatumia magari ya doria.

Mapema mwaka huu Rais Dk. John Magufuli aliliagiza Jeshi la Polisi kutumia mbinu za kisasa katika kukabiliana na uhalifu na kuifanya nchi kuwa sehemu salama nyakati zote.

Dk Magufuli alionesha kushangazwa na askari wa Jeshi la Polisi kunyang’anywa silaha yake na majambazi na wakati mwingine kuuliwa na majambazi, akihoji uwezo wa majambazi kiasi cha kuwatesa polisi kiasi hicho.

Rais alikuwa akizindua Mpango wa kuboresha usalama wa jamii na mali zao, ambao una dhamira ya kupunguza uhalifu ambapo ameliagiza jeshi hilo kuwahi kushughulikia majambazi kabla ya wenyewe kushughulikiwa na majambazi hayo.

Pamoja na hali hiyo Jeshi la Polisi lilitangaza mikakati mbalimbali ikiwamo ukaguzi maalumu wa bodaboda na kufunga kamera za CCTV katika miji mikuu ili kufuatilia matukio mbalimbali.

Majambazi hao ambao kwa muda sasa wamekuwa wakiibuka na mbinu mpya ikiwamo ya kutumia bodaboda kuvamia benki na wanaotoka benki na kuwapora fedha.

Licha ya polisi kuweka ulinzi maalumu na waendesha bodaboda watakaoonekana kupakia kitu chochote na kukiweka mbele (katika tenki la mafuta) au kiti cha nyuma, ikiwemo kusimamishwa na kupekuliwa  lakini bado mbinu hiyo imekuwa ikifeli na watu wakijikuta wakidhurika.

Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya wananchi kuvamiwa na kuporwa fedha, ikiwa ni muda mfupi baada ya kuzichukua benki huku wafanyakazi wa benki wakidaiwa kuhusika kutoa taarifa za wateja.

Mara zote majambazi hutumia bodaboda kufanikisha uhalifu huo, huku wakiwa na silaha ambazo huzitumia kutishia, kujeruhi na wakati mwingine kuua.

Chanzo: Mtanzania

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger