Hatua hiyo imekuja baada ya muimbaji huyo wa Aje kuonekana kuongoza kwa kura nyingi zilizopigwa na mashabiki kupitia mtandao wa tuzo hizo.
“Kiukweli mpaka sasa hivi mimi mwenyewe sijui ni kwa sababu gani, watanzania na mashabiki wote hawajui ni kwa sababu gani. Kama ulivyozungumzia na juhudi zilivyokuwa zikifanyika pale na watu walipiga kura kweli, kwa sababu watu wanavyokuwa wakipiga kura pale mabadiliko yanakuwa yanaonekana,” amekiambia kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.
“Kwa hiyo mashabiki walikuwa wanataka kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea at least tuweze kupata hata voice ya explanation kiundani ili kila mtu afahamishwe ni kitu gani au ni vigezo gani wametumia kufanya mimi nisishinde ile tuzo. Hiko ndio kitu tunachosubiria na menejimenti yangu.”
Muimbaji huyo alikuwa akiwania tuzo hiyo pamoja na wasanii wengine, akiwemo Olamide na Wizkid kutoka Nigeria na Black Coffee na Cassper Nyovest wa Afrika Kusini.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment