Nov 24, 2016

Huu Hapa Ushauri wa Mzee wa Upako Kwenda Kwa Rais Magufuli Kuhusu Wapinzani

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) lililopo Ubungo-Kibangu jijini Dar, Anthony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako, amemsihi Rais Dk. John Magufuli kuwa na utayari wa kusikiliza hoja muhimu za wapinzani.

Mzee wa Upako aliyasema hayo alipozungumza na gazeti hili wiki mbili zilizopita, alipokuwa akitoa maoni yake juu ya mwaka mmoja wa Rais Magufuli.

Alisema ni vema Rais  Magufuli akawa na utayari wa kusikiliza kelele za wapinzani kwa sababu baadhi yake zina hoja za msingi.

Mchungaji huyo ambaye ni miongoni mwa viongozi wa dini waliopata nafasi ya kutembelewa na Rais Magufuli Kanisani kwake alisema wanachama wenzake wa CCM hawawezi kumpigia kelele kutokana na uoga wa kushughulikiwa kisiasa, hivyo watu pekee wanaoweza kufanya hivyo ni upinzani.

Hata hivyo pamoja na kumshauri Rais, lakini pia aliwataka wapinzani kuwa na mipaka katika kusema ili kulinda masilahi ya nchi.

“Ila wapinzani pia waseme kwa mipaka ili kulinda masilahi ya nchi. Kila kitu kizungumzwe kwa wakati wake,” alisema.

Mbali na ushauri huo, lakini pia Mzee wa Upako alimwagia sifa Rais Magufuli kwa kufanya mambo mengi mazuri ndani ya kipindi chake cha mwaka mmoja ikiwa ni pamoja na kuwataka Watanzania waendelee kumwombea rais huyo kwa kuwa amethubutu kupambana na watu waliozoea kula kwa mikono na miguu bila kunawa.

Alisema Rais Magufuli amefanikiwa kurudisha nidhamu kwa watumishi wa serikali.

“Sasa watumishi wa umma wamekuwa na hofu ya kukiuka maadili ya utumishi, hata kama kuna mambo yanafanyika kinyume na sheria ni kwa kificho sana, kwa hiyo mwaka mmoja tumeona mabadiliko makubwa sana, nidhamu imerudi, pili ametimiza baadhi ya ahadi zake kama ile ya kutoa kila mwezi zaidi ya bilioni 28 kwa sekta ya elimu. Pamoja na hayo amehamasisha uchangiaji wa madawati tunaona imetimia, mwaka wa pili haya mengine yatatekelezeka.

“Pia kwa mwaka mmoja amefunga mianya mingi ya ufisadi, mishahara hewa, wafanyakazi hewa ameokoa mamilioni ya fedha, lakini kitendo cha kuchukua fedha za serikali kutoka benki binafsi na kupeleka Benki Kuu (BOT) ni hatua kubwa kuimariza uchumi na nguvu ya serikali kwa sababu serikali inaweka fedha benki inakopa fedha yake yenyewe inarudisha na riba, pia sheria ya manunuzi ya umma, ameivalia njuga na kuifanya kutokuwa mwanya kwa upotevu wa mapato ya serikali, pia ukusanyaji wa kodi na ukarabati mkubwa wa mwenendo wa bandari ya Dar es salaam, tumeona pia ameimarisha umoja na utulivu aliokuta,” alisema.

Alisema ingawa si sahihi kumpima kiongozi wa nchi maskini kama Tanzania kwa mwaka mmoja, ni dhahiri kuwa hatumtendei haki kwani ilipaswa kumpa walau miaka minne.

“Ila kuna mambo tunaweza kusema amethubutu amefanya hayo tunayaona. Namuomba aendelee hivyohivyo na Watanzania tumuombee Mungu ampe nguvu maana kupambana na majitu yaliyozoea kula kwa mikono na miguu tena bila kunawa si kazi ndogo. Kwa miaka hii mitano tutaona mabadiliko,” alisema.

Alisema Watanzania wasifedheheke  kutokana na sera za Rais Magufuli za kubana matumizi na kuzuia safari za nje kwa kuwa baada ya muda mfupi hali itakuwa shwari.

“Watu walikua wamezoea kusafiri ovyo, ilikuwa hakuna sababu ya kuwa na mabalozi nje ya nchi  kwa sababu safari zote walikuwa wanasafiri, lakini kitendo chake cha kufanya shughuli zote za nchi kushughulikiwa na mabalozi wawakilishi ni jambo zuri sana. Sasa watu walikuwa wanahamisha fedha kwenye mikono michafu… ndio wakati wa kuihamisha kutoka kwenye mikono hiyo hivyo watu wavumilie maumivu hiki ni kipindi cha mpito.

“Namsisitiza Rais akamate hapohapo baadaye fedha itatoka kihalali. Nafuu watu wawe na fedha chache halali ila si haramu, na kimsingi watu wanaosema fedha mtaani hamna ni waongo kwa sababu watu walikuwa hivihivi hamna anayesema alikuwa na fedha nyingi. Zaidi walikuwa wanazitumia hovyo kwenye mahoteli na mabaa.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger