Nov 28, 2016

Kiama Walioghushi vyeti Chawadia

KIAMA cha walioghushi vyeti ama kutumia vyeti vya watu wengine kwa lengo la kujitafutia ajira serikalini, kinakaribia baada ya Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), kubainisha kuwa liko katika hatua za mwisho za kukamilisha uhakiki wa vyeti vya watumishi hao.

Kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano ya mwaka 2004, ni kosa la jinai kughushi vyeti.

Akizungumza na gazeti hili kwa simu Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi, alisema mpaka sasa maofisa wa baraza hilo waliosambazwa mikoani kufanya uhakiki huo, wengi wao wamerejea na wachache waliobaki wanakamilisha kazi hiyo ili warejee Dar es Salaam.

“Ni kama mchakato wa uhakiki uko katika hatua za mwisho na kinachofanyika sasa ni kufanya majumuisho.

Siwezi kusema lini hasa tutamaliza, lakini kazi kubwa tumemaliza na kinachofanyika sasa ni majumuisho,” alisema Nchimbi.

Alisema utaratibu wa uhakiki huo wa vyeti ulianza rasmi Oktoba 10 na ulitarajiwa kukamilika Novemba 14, mwaka huu. Hata hivyo, alisema baada ya uhakiki huo wa vyeti, baraza hilo litawasilisha mrejesho wa matokeo ya uhakiki huo kwa taasisi husika zilizowasilisha vyeti vya watumishi wake kwa hatua zaidi dhidi ya watumishi watakaobainika kufanya udanganyifu.

“Sisi tunafanya uchambuzi wa vyeti hivi tulivyoletewa na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kuvihakiki, baada ya hapo tutatoa mrejesho kwa taasisi husika kuwa kati ya vyeti ilivyotuletea vingapi ni vya kughushi na taasisi hiyo ndio itakayochukua hatua,” alisema.

Hata hivyo, alifafanua kuwa kwa mujibu wa utaratibu wa Necta, mtu akifanya udanganyifu wa vyeti kwa kughushi au kutumia cheti kimoja kwa watu wawili, baraza hilo lina mamlaka ya kuwashtaki wahusika ikiwa ni pamoja na kumnyang’anya cheti mwenye cheti.

Alisema vyeti vyote vya kidato cha nne na cha sita vinavyotolewa kwa wahitimu ni mali ya Necta, hivyo endapo mtu akivitumia kinyume na inavyotakiwa baraza hilo lina mamlaka ya kumnyang’anya mhusika cheti hicho na kumshtaki.

Hivi karibuni, serikali ilitangaza rasmi kuanza kampeni ya kuwashughulikia na kuwaondoa katika utumishi wa umma watumishi wote walioajiriwa katika sekta hiyo wakitumia vyeti bandia.

Kutokana na kuanza kampeni hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano iliwataka watumishi hao waanze kujitathmini na kuanza kujiondoa wenyewe kabla ya kufikiwa na mabadiliko makubwa ya kusafisha sekta ya elimu na utumishi wa umma yanayokuja nchini.

Tayari Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki ameiagiza Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu (Utumishi) kuwachukulia hatua stahiki watumishi watakaobainika kutumia vyeti visivyo vyao ili kupata ajira serikalini.

Naye Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu (Utumishi), Leonard Mchau alisema ni kosa la jinai kughushi vyeti kwa lengo la kujipatia kazi, hivyo endapo mtu atagundulika ameghushi vyeti atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi.

Hata hivyo, tayari kuna baadhi ya taasisi zimebainika kuwa na watumishi walioghushi vyeti ikiwemo Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ambayo ilihakiki watumishi 704 na kati yao 219 waligundulika kuwa waliajiriwa kwa vyeti vya kughushi.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger