1. Kwa Kazi Hii Nzuri Anayofanya Rais Wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, Hivi Kweli Tanzania, Tuna Haja tena ya Kufanya Uchaguzi Wa Rais kwa mwaka 2020?.
2. Hatuwezi kufanya uchaguzi wa wabunge tuu na madiwani, na badala yake , ili kuokoa pesa, mali na muda?, na Magufuli apewe tuu a walkover ya kuendelea hadi 2025?!.
3. Au kwa vile Uchaguzi wa Rais ni takwa la kikatiba, hivyo uchaguzi huo lazima tuu ufanyike hata kama ni wastage of time, money and resources?!.
4. Na hiyo 2025 tukimuona bado anaweza, na anatufaa, kuna ubaya kuibadili katiba yetu tumpatie extension ya kutosha kuinyoosha Tanzania?!.
5. Kwani katiba ni nini?,si ni kipande tuu cha karatasi?!, nini muhimu kati ya kipande cha karatasi na umuhimu wa Magufuli kwa taifa?!.
6. Na Katiba ni ya nani?!, ni yetu?!, na iko kwa manufaa ya nani?!, si ipo kwa manufaa yetu?!, hivyo sisi ndio muhimu kuliko katiba, tukimtaka Magufuli, si tunaweza kuiweka tuu katiba pembeni?!.
7. Sasa kama Magufuli anatufaa sana, na katiba haitamruhusu kuendelea baada ya 2025, kuna ubaya gani kuibadili katiba kwa manufaa yetu?!,
8. Au kwani Katiba ni Msahafu kusema haiwezi kubadilishwa?!.
9. Na jee ubaya wowote wapinzani wa Tanzania mkiamua kwa kauli moja msisimamishe tena mgombea urais, na badala yake CCM ndio iwe inatoa rais siku zote kufuatia long eksipirience ya uzoefu wa muda mefu kwenye urais?.
10. Na kufuatia somo la urais wa Zanzibar, na kilichofanyika kwenye urais wa JMT, kweli wapinzani makini bado watahitaji kweli kusimamisha mgombea kushindana na Magufuli?!, kutakuwa ni kugombea au kujifuahisha tuu?!, au hata ikitokea ameshinda atatangazwa?!.
Hayo ni maswali tuu nimeanza kujiuliza aloud?!.
Jee wewe una maoni gani kuhusu hoja zangu hizi?!.
Paskali
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment