Nov 28, 2016

Maalim Seif Asema Polisi Wanambeba Lipumba

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amelituhumu Jeshi la Polisi kwa kubariki hujuma zinazofanywa na Profesa Ibrahimu Lipumba kwa kushirikiana na wafuasi wake kuvuruga chama.

Maalim Seif amemuandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akimuomba achukue hatua dhidi ya watendaji wake  wanaobariki hujuma hizo.

Alisema hayo jana alipozungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu changamoto zinazokipitia chama hicho.

“Chama kinakabiliwa na changamoto nyingi katika kutekeleza majukumu yake kutokana na vitendo vya hujuma vinavyofanywa na Profesa Ibrahimu Lipumba (Bwana yule) na wafuasi wake kwa msaada wa Jeshi la Polisi.

“Jeshi la Polisi limekua likivamia na kuvuruga mikutano halali ya chama cha CUF.

“Matukio yako mengi lakini nayataja haya baadhi, Lipumba na kundi lake alivamia  mkutano mkuu maalum wa chama  na kuuvuruga Agosti 21 mwaka huu katika Hoteli ya Blue Pearl, uliogharimu Sh milioni 600.

“Utekaji wa wanachama na viongozi unaofanywa na makundi ya Profesa Lipumba pamoja na kuripotiwa bado hakuna kilichofanywa,” alisema.

Alitaja matukio ya uvamizi wa ofisi za chama Bagamoyo ambazo zilivunjwa na kuweka kufuli mpya kuzuia kazi za chama zisiendelee.

“Wabunge wetu walizuiliwa kufanya mikutano ya ndani lakini Bwana yule (Profesa Lipumba) anapewa kibali na Jaji Mutungi alimuandikia barua na nakala kwa IGP ili Jeshi la Polisi litoe ulinzi  katika mikutano yake maeneo mbalimbali,”alisema.

Alisema pamoja na kutolewa taarifa za matukio yote ya utekaji na uharibifu unaofanywa na wafuasi wa Lipumba bado jeshi hilo limekaa kimya.

Alisema CUF iliamua kuchukua hatua kwa kumtafuta Waziri Nchemba lakini hakupatikana kutokana na majukumu yake lakini wamemuandikia barua.

“Nimemuandikia Mwigulu barua Novemba 24 mwaka  huu yenye kumbukumbu CUF/HQ/AKM/2016/vol/000 kuelezea matendo yanayofanywa na watendaji wake ili achukue hatua zinazostahili.

“Inashangaza kuona Jeshi la Polisi linashirikiana na wahalifu, linalinda wahalifu wasifikishwe mbele ya sheria.

“Jeshi la Polisi limeshindwa kutekeleza majukumu yake kwa weledi, linaingilia shughuli za siasa.

Lipumba alijiuzulu kwa matashi yake mchana kweupe, pamoja na kushauriwa sana na viongozi wa chama na dini alikataa kata kata,”alisema Maalim.

Alisema hujuma zote zinazofanywa zinahusiana na harakati za kudai haki Zanzibar na kuna ushahidi wa mazingira kwamba dola imo ndani yake.

“Wanataka niendelee na mgogoro niache kudai haki, mimi na Lipumba hatuna ugomvi, ugomvi uliopo ni kati ya Lipumba na chama, hata tukikutanishwa leo siwezi kubatilisha uamuzi wa Baraza Kuu.

“Lipumba bado hajasema sababu za kujiuzulu, awaambie Watanzania asiruke ruke,”alisema na kuongea kwamba yuko tayari kufanya mdahalo na Profesa Lipumba.

Maalim Seif alisema  kutokana na kuonyesha msimamo dhidi ya dhuluma inayofanywa na Profesa Lipumba na Serikali dhidi ya CUF, Msajili amezuia ruzuku.

“Kuanzia Agosti 2016 Msajili hajatoa ruzuku ya CUF kwa maelezo kuwa chama kina mgogoro wakati alitaka kumpa Lipumba,”alisema.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger