Nov 7, 2016

Msimamo wa Rais Magufuli Kuhusu Katiba Mpya Wamtesa Tundu Lissu

Siku tatu baada ya Rais John Magufuli kueleza bayana kwamba suala la Katiba Mpya si kipaumbele chake kwa sasa akitaka aachwe ili ainyooshe nchi kwanza, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amesema kiongozi huyo hawezi kunyoosha nchi bila kuwa na Katiba Mpya iliyotokana na maoni ya wananchi.

Wakati Lissu akisema hayo, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damiani Lubuva amesema atatolea ufafanuzi suala hilo siku za karibuni.

Lubuva na Lissu walieleza hayo walipotakiwa kuzungumzia kauli ya Rais Magufuli kwamba kipaumbele chake ni kuchapa kazi ili kuinyoosha nchi na mengine yafuate ikiwamo Katiba Mpya.

Magufuli alitoa kauli hiyo Novemba nne, alipozungumza na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari siku moja kabla ya kutimiza mwaka mmoja tangu aingie madarakani.

Lakini, Lissu alisema nchi haiwezi kunyooka bila kunyoosha kwanza Katiba inayoiongoza ambapo alipendekeza uwepo wa Katiba Mpya badala ya kuifanyia marekebisho iliyopo sasa.

“Tulishaondoka kwenye mjadala wa kuziba viraka kwenye Katiba, tumeshakubaliana kwamba tunahitaji mabadiliko ya Katiba yote si sehemu tu. Rais asidhani mtu akikalia kiti hicho basi neno lake ni sheria ya nchi. Haiwezekani,” alisema.

Alisema mchakato wa Katiba Mpya hautakiwi kuendelea ulipoishia kwa maelezo kuwa ikiwa hivyo nchi haiwezi kufika popote.

“Katiba Inayopendekezwa ni kama imepakwa rangi ya Katiba ya sasa. Inaonekana mpya lakini misingi yake ni ya Katiba ya sasa…, kama Rais Magufuli anataka kunyoosha nchi, anapaswa kuirejea Rasimu ya Jaji Warioba. Tuanzie hapo, zaidi ya hivyo atajidanganya na kuwadanganya Watanzania,” alisema.

Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki alisema nchi haiwezi kuongozwa kwa matamko ya kiongozi mkuu pekee bila kuangalia matatizo ya kisheria.

“Anafikiri akiamua yeye kama Rais unafuata utekelezaji? Kuna matatizo mengine ya kikatiba…, hayawezi kubadilika bila kufanyika kwa mabadiliko ya Katiba. Kuna mambo ili yanyooke ni lazima uwe na Katiba nzuri. Usipoyashughulikia hayo mengine yote hayatawezekana,” alisema Lissu.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ,Jaji Lubuva alipoulizwa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya na kauli ya Rais Magufuli alisema suala hilo linahitaji kukaa na kulizungumza vizuri.

“Naomba upokee kuwa nimekuelewa ila kwa sasa ninachoweza kusema nitatoa ufafanuzi mzuri kuhusu suala hilo kwani ni jukumu la ofisi yangu,” alisema.

Alisema ni kweli baada ya Katiba Inayopendekezwa kupigiwa kura na Bunge hatua iliyokuwa inafuata ilikuwa ni kuitisha Kura ya Maoni, lakini ilishindikana kutokana na kuingiliana na Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.

Kabla ya Rais Magufuli kutoa kauli yake kuhusu Katiba Mpya, siku za karibuni NEC iliwahi kueleza kwamba ipo katika hatua mbalimbali za kuhakikisha mchakato huo unafanyika kwa mujibu wa sheria.

Katika kauli yake ya Novemba nne, Rais Magufuli alisema wakati anaomba kura hakuweza kuzungumzia Katiba hivyo kwa sasa kilichopo mbele yake ni kunyoosha nchi kwanza na Katiba mpya itakuja baadaye.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

1 comment:

  1. Njaa kali sana ni sawa na mwenzake Lema yaani hao wawili ni elements in oue society mnaonaje???
    Sheria gani anajua huyu mtu aliyesoma ku-pass mtihani???? hahahhhhh

    ReplyDelete

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger