KOCHA wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema kwamba refa Rajab Mrope wa Ruvuma alilikubali bao la pili la Mbeya City jana baada ya ushauri wa Kamanda wa Polisi Mbeya, Dhahiri Kidavashali.
Akizungumza leo mjini Mbeya, Pluijm alisema kwamba halikuwa bao halali na refa alikwishalikataa awali, lakini kwa agizo la Kidavashali akalikubali.
“Bao la pili lilikuja baada ya mpira wa adhabu tena. Refa aliwarudisha nyuma wachezaji wetu na kuwaambia wasubiri filimbi na wakati huo huo bila filimbi ya refa wakapiga mpira wa adhabu na kufunga ikawa 2-0,”.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment