Nov 13, 2016

Serikali Haina Idadi ya Watanzania Watakaotimuliwa na Trump Marekani

Serikali imesema kuna Watanzania wengi wanaoishi Marekani kinyume cha sheria, lakini haijui idadi yao wakati Rais mteule wa nchi hiyo, Donald Trump akisubiriwa kutekeleza ahadi yake ya kutimua wahamiaji haramu.

Kuchaguliwa kwa Trump kuwa Rais wa 45 wa Taifa hilo kubwa, kumeibua hofu miongoni mwa kwa mataifa mbalimbali kuhusu raia wao wanaoishi bila ya nyaraka halali kutokana na sera za mfanyabiashara huyo maarufu za kutotaka wageni haramu.

Awali, Serikali ya Rais Barack Obama ilitoa ahueni kwa watu wanaosadikiwa kuwa milioni 11.1 (kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2014 za taasisi ya utafiti ya Pew ya Marekani) baada ya kuwaruhusu kupitia mchakato ambao ungewapa uhalali wa kuishi nchini humo.

Lakini katika kampeni zake, Trump alisema hahitaji wageni walioingia Marekani kwa kukwepa sheria na hivyo atawatimua ili wakaanze mchakato wa kuomba kuingia Marekani wakiwa kwenye nchi zao.

Akizungumza na Mwananchi juzi, Kaimu Mkuu wa Idara ya Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje, Robi Bwiru alisema: “Kuna idadi kubwa ya Watanzania wanaoishi Marekani lakini kwa kuwa suala la mtu kutaka kutambulika na ubalozi wake ni la hiari, hatuna idadi kamili ya Watanzania ambao wapo kule bila nyaraka halali.”

Kuhusu misimamo ya kiongozi huyo kutoka chama cha Republican dhidi ya nchi za Afrika, Bwiru alisema Tanzania haiwezi kutoa msimamo wowote kabla ya kuona utekelezaji wa ahadi zake.

Kwa mujibu wa taasisi ya utafiti ya Pew, Wamexico ndiyo wanaoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wageni wanaoishi bila ya nyaraka halali wakiwa asilimia 52, lakini kutokana na uchumi wa Mexico kuimarika pamoja na ulinzi mkali mpakani, idadi yao inapungua.

Badala yake, watu kutoka Kusini mwa Jangwa la Sahara, ikiwamo Tanzania, wameongezeka katika kipindi cha miaka sita iliyopita.

Pew inakisia kuwa idadi ya wageni kutoka Afrika wanaoingia isivyo halali imeongezeka hadi kufikia asilimia 37.5, wakati kutoka barani Asia imeongezeka hadi asilimia 11.5 na kutoka Amerika ya Kati ni asilimia 6.3.

Pew inaeleza kuwa sababu za kuongezeka kwa wahamiaji haramu ni vurugu Afrika ya Kati na ukosefu wa ajira barani Asia na Afrika.

Katika kampeni zake, Trump alisema atatekeleza msimamo wake wa kuwarejesha wahamiaji haramu, ikiwa ni pamoja na kujenga ukuta kwenye mpaka wa nchi hiyo na Mexico.

“Nitaanzisha kikosi maalumu cha kuwafukuza wahamiaji nchini. Kazi yake kuu itakuwa ni kuwasaka na kuwarejesha walipotoka wahamiaji haramu walioingia Marekani kwa kukwepa sheria za nchi, kama alivyozikwepa Hillary Clinton, pengine naye watamfukuza,” alisema Trump.

Aliongeza kuwa ujumbe wake kwa ulimwengu mzima ni kwamba haiwezekani kupata uraia wa Marekani kwa kuingia nchini humo kinyume na sheria.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger