Nov 20, 2016

Watumishi 71 Waitapeli Serikali Mil. 840/-


WIMBI la watumishi hewa limechukua sura mpya mkoani Arusha baada ya kubainika kuwa kuna majina ya wafanyakazi waliokwenda masomoni lakini hawajaonekana kwenye vyuo walivyodaiwa kusajiliwa na wala hawapo kwenye sehemu zao za kazi ingawa wanaendelea kupokea mishahara yao ya kila mwezi.

Hii ni kutokana na mishahara yao kuendelea kuingia kwenye akaunti zao benki pamoja na malipo ya kuhudhuria mafunzo kwenye vyuo ambavyo ingawa vimepokea fedha za ada na huduma nyingine, hazijapokea wafanyakazi hao ambao walitakiwa kujiunga na masomo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, tayari kuna wafanyakazi 71 wa halmashauri za Meru na Arusha Vijijini, walioaga kwenda masomoni katika vyuo tofauti nchini, lakini imebainika kuwa hawapo kwenye vyuo hivyo.

Mnyeti akizungumza na gazeti hili jana alisema kati yao, 15 ni wale waliotakiwa kujiunga na vyuo mbalimbali na idadi yao kwenye mabano, Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (1), Chuo Kikuu cha Mount Meru (6), Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (6), Chuo Kikuu cha Mwenge (6); Chuo cha Eckinford Tanga (5) na Chuo cha Tiba cha KCMC Moshi (4).

Wengine Chuo Kikuu cha Arusha (3), Chuo cha Ualimu cha Patandi (3), Chuo Kikuu cha Ruaha (3), Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere Memorial (3) na Chuo Kikuu cha Kampala (3).

Wapo pia waliotakiwa kuwepo katika Chuo cha Tanzania Institute of Accountancy (1), Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (2), Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa (2), Chuo Kikuu cha SAUT-Mbeya (1), Chuo Kikuu cha Jordan (1), na Chuo Kikuu cha Stephano Memorial Moshi (1), hivyo kufanya jumla yao wote ifikie wafanyakazi 71.

Alisema walioomba kwenda kusoma kutoka wilaya ya Arumeru ni wafanyakazi 306, lakini kati yao 71 hawajaonekana kwenye vyuo hivyo na kwamba inasadikiwa walisingizia kwenda kusoma tangu mwaka 2011 lakini wako kwenye shughuli nyingine ikiwemo kuajiriwa kwenye kampuni nyingine binafsi pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Alisema kwa kitendo hicho wafanyakazi hao wameiingizia serikali hasara ya Sh 837,545,280/- (karibu Sh milioni 840) kupitia mishahara ambayo ilikuwa ikiendelea kuingia kwenye akaunti za benki za wafanyakazi huku wakiwa katika ajira sehemu nyingine kwa kisingizio cha kwenda kusoma.

Kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkuu huyo wa Wilaya, Alexander Mnyeti alitoa siku 30 kwa wafanyakazi wote 71, warudishe fedha zote za mishahara waliyokuwa wakipokea wakidai kuwepo masomoni kumbe wapo katika ajira nyingine za nje.

Pia aliwataka wafanyakazi wengine wote ambao wako masomoni warudi kutoa taarifa za maendeleo ya masomo huko waliko kwa waajiri wao ili serikali ijiridhishe kuwa kweli wanasoma na wanaendelea vizuri.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Christopher Kazeri alisema kuna haja ya uongozi kufuatilia watumishi wanaoomba ruhusa kwenda masomoni maana wengi ni waongo, wanaitapeli serikali wakijua wazi wanakwenda kufanya shughuli zao, na hasa kipindi hiki ambapo kuna upungufu wa watumishi wa umma.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger