Dec 8, 2016

CUF ya Lipumba, Maalim Seif Vita Mpya

Mgogoro wa uongozi unaoendelea ndani ya chama cha CUF huenda ukaathiri ushiriki wake kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Januari 27 baada ya pande zote mbili zinazosigana kujiandaa kuteua wagombea.

Mbali ya mgogoro huo kuhofiwa kukiathiri chama pengine hadi kusababisha wagombea wake kuzuiwa, pia unaweza kuudhoofisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Habari kutoka ndani ya chama hicho zinasema upande wa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Msajili wa vyama vya siasa uko kwenye maandalizi ilhali ule wa Katibu Mkuu, Seif Sharrif Hamad unatarajiwa kukutana na watendaji wa chama kujadili ushiriki wao.

Profesa Lipumba aliyeiongoza CUF tangu mwaka 1995, alijiuzulu kwa hiari uenyekiti wake Agosti 2015 lakini siku chache kabla ya CUF kuitisha mkutano Agosti mwaka huu wa kujadili barua yake, aliandika barua ya kutengua kujiuzulu na akarejea kazini.

Siku ya mkutano mkuu uliofanyika Ubungo Plaza, wajumbe waliridhia kujiuzulu kwake lakini walipoingia kuchagua mrithi wake, wafuasi wa Profesa Lipumba walivamia mkutano na kuuvuruga hali iliyosababisha baadaye kusimamishwa kwake.

Alipoulizwa jana namna CUF yenye mgogoro itakavyoshiriki uchaguzi wa madiwani katika kata 22 Bara na ubunge wa Jimbo la Dimani, Zanzibar, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF, Julius Mtatiro alisema wapo katika mikakati kuhakikisha wanashiriki kikamilifu.

Mtatiro alisema muda wowote kuanzia sasa Katibu Mkuu, Maalim Seif atakutana na watendaji wa chama kujadili kwa kina suala hilo na kutoa maelekezo.

“Tutashiriki vizuri na niwaweke wazi Watanzania kuwa shughuli za chama zinaendelea kama kawaida hivyo kamati za utendaji zitatimiza wajibu wake wa kuwapitisha wagombea watakaojitosa kwenye kinyang’anyiro,” alisema.

Kuhusu Profesa Lipumba, Mtatiro alisema, “Hatuwezi kufanya kazi na mtu wa CCM kumsogeza karibu yetu ni kumleta atuharibie chama jambo ambalo hatuwezi kuliruhusu. Ingekuwa lile suala la kujiuzulu aliteleza tungemwelewa na kumsamehe lakini inavyoonekana yupo kwenye mipango yake katu hatuwezi kumuweka karibu.”

Lakini Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF anayemuunga mkono Lipumba, Abdul Kambaya alisema, “Tuna kikao leo (jana) upande wa Bara chini ya Mwenyekiti Profesa Lipumba kujadili suala hilo la uchaguzi, kuhusu upande wa Zanzibar sifahamu chochote.”

Akizungumzia uchaguzi huo mdogo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema upande wa Zanzibar, Salum Mwalimu alisema Ukawa utakuwa bega kwa bega na CUF katika uchaguzi huo kwani wanaitambua kuwa iko moja si mbili kama inavyotengenezwa na watu wasiopenda maendeleo ya chama hicho.

“Tunatambua na kuheshimu uamuzi wa wanachama na viongozi halali wa chama, CUF iko moja, kama kuna mtu anatengeneza propaganda alifanya hivyo akiamini anakwenda kukiua chama ajue bado kinaendelea kusimama,” alisema.

“Pale atakaposimamishwa mgombea kutoka chama hicho Ukawa tutamuunga mkono na kumpigania kuhakikisha anashinda. Tunaamini pia nao watafanya hivyo akisimamishwa mgombea wa Chadema, ”alisema Mwalimu

Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi Juju Danda alisema mgogoro wa CUF hautaleta changamoto yoyote kwenye Ukawa kwa kuwa wanamtambua katibu mkuu. Alisema Ukawa unamtambua Maalim Seif na ndiye mtendaji mkuu wa chama hivyo watakuwa tayari kushirikiana naye katika kila jambo.

Kuhusu mpasuko unaoendelea ndani ya chama hicho, Danda alisema suala hilo waachiwe CUF wenyewe ndiyo watakaoamua. “Mtendaji Mkuu wa chama ni katibu si Mwenyekiti, na kwa kuwa tupo pamoja na Maalim hatuoni changamoto yoyote yeye ndiye anayesimamia uteuzi na tunategemea mambo yatakwenda sawa,” alisema.

Katika hatua nyingine hatima ya Jaji Sekieti Kihiyo anayesikilkiza kesi ya CUF kujitoa sasa itajulikana Desemba 14 atakapotoa uamuzi wa maombi ya wadai kumtaka ajiondoe.

Jaji Kihiyo alipanga kutoa uamuzi wa maombi hayo dhidi yake jana baada ya kumaliza kusikiliza hoja za pande zote katika kesi hiyo, ambazo zilizua mvutano mkali baina ya mawakili wa wadai kwa upande mmoja na mawakili wa wadaiwa pamoja na Jaji Kihiyo kwa upande mwingine.

Kesi hiyo imefunguliwa na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wadhamnini wa CUF, dhidi ya Profesa Lipumba, Naibu Katibu Mkuu wa chana hicho Bara, Magdalena Sakaya pamoja na wanachama wengine tisa waliosimamishwa uanachama wa chama hicho.

Wengine ni Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, ambaye ndiye mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), ambaye ni mdaiwa wa pili.

Kesi hiyo ilitarajiwa kusikilizwa jana lakini kabla ya kuendelea, kiongozi wa jopo la mawakili wa wadaia, Juma Nassoro aliieleza mahakama kuwa wadai wameandika barua wakimtaka jaji ajiondoe kuendelea na kesi hiyo kwa maelezo hawana imani naye.




Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger