Wafuasi hao ni wa Bodi ya Wadhamini ya chama hicho wanaomuunga mkono Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na wanaomuunga mkono Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii, Dk Benson Bana alisema kuwa kesi inapokuwa mahakamani kinachotafutwa ni haki na kwamba hasira zao sio suluhisho.
Dk Bana alisema wamekuwa wakikemea masuala hayo kwa kuwa siasa za kitanzania haziko namna hiyo.
“Kitendo cha kupigana mahakamani ni cha kihuni na utovu wa nidhamu. Watu wanatakiwa kutii sheria wawapo mahakamani na kuwa na nidhamu. Hali iliyotokea imewajengea mazingira kwamba wao hawatii sheria zilizowekwa,’’ alisema Dk Bana.
Alifafanua kuwa wenye dhamana ya kusuluhisha ugomvi huo ni viongozi wakuu wa chama hicho, akiwemo Profesa Lipumba na Maalim Seif kwa kutumia busara walizonazo.
Alisema viongozi hao wanatakiwa kuandaa mazingira mazuri ya kukaa chini kuzungumza na kwamba ugomvi na malumbano hayatakisaidia chama hicho badala yake hakutakuwa na demokrasia inayotakiwa.
Kwa mujibu wa Dk Bana, chama hicho kinajichafulia haiba yake ambayo endapo watatafuta upenyo wa kusuluhisha suala hilo kupitia pande zote, hakutakuwa na malumbano.
‘’Kisiasa haitakiwi kugombana na wala sio utamaduni wa watanzania kupigana kwa sababu tayari kesi hiyo ipo mahakamani na ni lazima wazingatie sheria kwa kusubiri uamuzi wa mahakama,’’ aliongeza.
Wafuasi hao wa CUF walifanya tukio hilo kabla ya kuingia kwenye chumba cha mahakama tayari kwa kusikiliza uamuzi wa kujitoa au kuendelea kwa Jaji Sekiet Kihiyo kusikiliza kesi hiyo na baada ya kutoka mahakamani.
Katika vurugu hizo, watu watatu akiwemo Robert Samson alijeruhiwa na shingoni kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kinachodhaniwa kuwa ni kisu.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment