Feb 7, 2017

Kauli Walizotoa Viongozi Kumi Kuhusu Vita Dhidi ya Madawa ya Kulevya

“Katika vita hii ya madawa ya kulevya, hakuna cha mtu aliye maarufu, hakuna mwanasiasa, hakuna askari, hakuna waziri au mtoto wa fulani ambaye akijihusishwa aachwe. Hata kama angekuwa mke wangu Janeth, akijihusisha shika.”

Paul Makonda (Mkuu wa Mkoa, Dar es salaam

“Haya mapambano si ya mtu mmoja na kelele nyingine mnazozisikia zinatupa hamasa tuendelee kufanya kazi. Tunachotafuta sisi ni majibu, tukifika mbinguni tumweleze Mungu kwamba dhamana uliyotupa tuliitendea haki.”

Nape Nnauye (Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo)

“Ni muhimu kulinda haki ya mtuhumiwa. Jambo lenye mjadala ni busara inayotumika kushughulika na wahusika ili kusaidia vyombo vyengine kuwataja wanaosambaza. Tusiwahukumu kwa tuhuma maana wasanii kujenga ‘brand’ (jina) ni kazi kubwa ila kubomoa jina ni sekunde tu. Ni vizuri tukaangalia, tufanye katika namna ya kumlinda mtuhumiwa ili hata kama hahusiki jina lake lisiporomoke.”

Kamishna Simon Siro (Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es salaam)

“Hata hao wanaosema wana ‘brand’ kubwa wamejitahidi kutoa ushirikiano na wako waliokamatwa na vielelezo, wengine wamekiri kutumia na wametusaidia sana kwenda kuwakamata wanaouza. Nimejitahidi mwenyewe kuwahoji mmoja mmoja, niliona kuwapa wapelelezi wawahoji wanaweza wasitende haki…mimi ni kachero mzoefu.”

Esther Bulaya (Mbunge wa Bunda Mjini)

“Namshauri mdogo wangu Makonda, hao anaowakamata na kuwaweka ndani ni watu wadogo sana, badala yake awakamate mapapa ambao ndio wanaoingiza dawa hizo. Makonda akamuone mama Leila kule gerezani, akamueleze dawa zinavyoingizwa nhini kwa sababu hao anaowakamata ni wale wanaotakiwa kuwa Mwananyamala au Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu.”

Goodluck Mlingwa (Mbunge wa Ulanga)

“Wafanyabiashara wa madawa ya kulevya hamna asiye wajua, tuna wajua. Humu ndani wapo, nje ya Bunge wapo.”

Joseph Msukuma (Mbunge wa Geita Vijijini)

“Kwa nini vyombo vya dola visimchunguze Makonda maana anasafiri sana Ulaya na Dubai, hivi anasafiri kwa mshahara upi alionao? Kama Rais Magufuli amesema kama mkewe Mama Janeth anahusika na dawa za kulevya akamatwe, kwanini Makonda naye asihojiwe kwa sababu amewapangishia watu nyumba wakati wanajihusisha na dawa za kulevya?”

Halima Mdee (Mbunge wa Kawe)

“Hapa tusitafute ‘headline’ kwenye vyombo vya habari, lazima tuwe na ‘political will’ (utayari wa pamoja wa kisiasa), tuache usanii. Kama mheshimiwa Rais hawajakwambia, basi ujue kwenye kampeni zako ulichangiwa na hao wauza dawa za kulevya. Nchini sasa tuna njaa, kwahiyo mnachotaka kufanya ni kubadili akili za Watanzania kwa hizi mbwembwe zenu. Mnasema Wema Sepetu anahusika na dawa za kulevya wakati alizunguka na Makamu wa Rais kwenye kampeni  kwa miezi yote mitatu.”

Hussein Bashe (Mbunge wa Nzega Mjini)

“Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete alisema anayo orodha ya wafanya biashara wa dawa za kulevya. Kwakuwa alisema anayo, namuomba Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi amfuate Kikwete pale kijijini kwake Msoga ampe hiyo orodha ili waungane na kasi ya Makonda ya kupambana na dawa hizo. ”

Zitto Kabwe (Mbunge wa Kigoma Mjini)

“Ukiona kifaranga kipo juu ya chungu ujue chini kuna mama yake, leo Rais ametamka kuwa vita ile sio ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam peke yake bali ni vita ya wote. Vita ya wote kuendeshwa na Mkuu wa Mkoa mmoja ni jambo la kushangaza kidogo, lakini halina ubaya kwani lazima awepo wa kubutua kombolela.”


Share:

Serikali Kupiga Marufuku Pombe za Viroba....

Serikali inatarajia kupiga marufuku utengenezaji na uingizaji wa pombe za bei rahisi maarufu kama “Viroba” Nchini, ndani ya miezi mitatu ijayo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Hamisi Kigwangalla ameyasema hayo leo Bungeni, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu hoja za wabunge waliokuwa wakilalamikia  kilevi hicho kinavyopunguza nguvu kazi ya Taifa, wakati wa uwasilishwaji wa taarifa za kamati ya kudumu ya Bunge ya masuala ya Ukimwi pamoja na Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa mwaka 2016/17.

Dkt. Kigwangalla amesema kuwa baada ya miezi mitatu kilevi hicho kitapigwa marufuku kutengenezwa au kuingizwa nchini pamoja na kuziba mianya yote ya uingizaji wa kilevi hicho ambacho kimekuwa kikitumiwa na vijana wengi, hivyo kuharibu nguvu kazi ya Taifa.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Esther Matiko amesema kwamba pombe hiyo inasababisha vifo vya vijana wengi nchini ambao ndio tegemeo kubwa na nguvu kazi ya Taifa.

“Katika kipindi hiki kifupi cha likizo yangu, nilikuwa jimboni kwangu na tumezika vijana wanne ambao wamefariki kutokana na matumizi ya viroba. Hivyo wananchi wa jimbo langu wameniagiza kuja kulieleza Bunge athari za pombe hiyo ili tuweze kujadili na kuona namna gani  ya kuliokoa Taifa hasa vijana kutoka katika janga hilo,” alifafanua Matiko.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Kamati imebaini uwepo wa uhusiano mkubwa kati ya matumizi ya pombe hizo na kuongezeka kwa tabia hatarishi zinazochangia ongezeko la vijana katika matumizi ya dawa za kulevya.

Aidha amesema kuwa hali hiyo inaathiri ufanisi wa nguvu kazi ya Taifa kutokana na madhara ya matumizi ya dawa za kulevya. Hivyo Kamati imeishauri Serikali kufungia kabisa uzalishaji na uuzwaji wa pombe hizo za viroba ili kulinusuru Taifa.


Share:

Serikali Kuwashushia Rungu Mashoga Vinara

Wakati wauza unga wakihaha kutafuta sehemu za kujificha kuukwepa moto wa mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda, siku za mashoga vinara nazo zimeanza kuhesabika.

Vita dhidi ya mashoga hao imetangazwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr. Hamis Kingwangala, jana.

“Naagiza James Delicious, Kaoge Mvuto na Dani Mtoto wa Mama wafike wenyewe Central Police Dar es salaam kwa mahojiano kabla hawajatafutwa,” aliandika kwenye Twitter.

Mashoga hao ni maarufu kwenye mitandao ya kijamii na wamejikusanyia mashabiki wengi.


Share:

Vita dhidi ya dawa za kulevya: Makonda atoa siku 10 kwa wahusika kujisalimisha

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa siku 10 kwa wenyeviti wa mtaa mkoani kwake kuwataja watu wanaowahisi wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Wito huo pia ni kwa watu wote wanaohusika kwenye biashara hiyo haramu pamoja na wazazi kuwasalimisha watoto wao.


Mkuu wa Mkoa huyo ameyasema hayo Jumatatu hii katika kituo kikuu cha Polisi Dar es Salaam akiongea na waandishi wa habari.

“Natoa siku 10 kwa kila Mwenyekiti wa Mtaa kwenye mitaa yote Dar es salaam kutoa taarifa za mtaa wake juu ya dawa za kulevya. Natoa siku 10 kuanzia kesho kwa Wazazi, kama wewe ni mzazi unaishi na mtoto anatumia dawa za kulevya na unaishi naye, njoo utoe taarifa tukikukamata baada ya siku kumi na mwanao anahusika tutaamini na wewe ulikuwa sehemu ya kumfanya mtoto wako atumie dawa za kulevya.”

Ameongeza, “Natoa siku 10 kwa Wafanyabiashara na Watumiaji wa dawa za kulevya, waje wenyewe Polisi kwa kamishna, kama umekuwa ukifanya biashara ya dawa za kulevya na umeacha njoo Polisi, nguvu tunayo, uwezo tunao hakuna kiunga tutashindwa kufika, hizi kelele nyingine zinatupa hamasa.”


Share:

Halima Mdee Amtetea Wema, Mlizunguka Naye Miezi 3 Kwenye Kampeni Hamkujua Anatumia Unga?

Wabunge wa upinzani Jumatatu hii wameikosoa vikali njia aliyoitumia mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika kupambana na biashara ya dawa za kulevya kwa kuwajumuisha mastaa wakiwemo Wema Sepetu kwenye orodha yake.

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amedai kuwa kinachofanyika ni ‘usanii’ kwakuwa anaamini Makonda anawajua vyema mapapa wa biashara hiyo wanaotakia kutajwa na sio kuwakamata akina Wema.

Mdee alimuingiza pia Makonda kwenye picha na kuikosoa safari yake ya siku 20 nchini Marekani huku akihoji nani aliifadhili. “Hakuna anayejua aliyemfadhili kwa siku 20, hana ubavu wa kuishi Marekani siku 20. Inawezekana hawa wauza unga ndio wanampeleka huko, anakuja anawakamata akina Wema, Wema kweli?”

“Alizunguka na nyie kwenye kampeni mlikuwa hamjui? Alikuwa na makamu wa Rais, miezi mitatu sijui mama na mtoto, mkapata kura za mateenagers kupitia huyo mtoto, kwahiyo siku zote kumbe ananusa kitu kama wa rais hajui!”

Wabunge wengine wa upinzani nao wamekosoa njia iliyotumika.


Share:

Jan 17, 2017

Serikali Yamalizana Na Wenyeviti Wa Serikali Za Mitaa, Yawaruhusu Kutumia Mihuri Yao

Baada ya mvutano wa muda mrefu baina ya Serikali na Wenyeviti wa Serikali za mitaa,Serikali imesitisha muongozo wake wa kuzuia kutumia mihuri kwa wenyekiti wa serikali za mitaa.

Akizungumza leo hii Jijini Dar es salaam na wawakilishi kutoka serikali za mitaa, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, George Simba Chawene amesema amesitisha muongozo uliotolewa juu ya utumiaji wa mihuri kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa mpaka hapo baadae itakapojadiliwa tena.

''Hakukuwa na dhamira yeyote ya kupunguza mamlaka ya heshima yenu Wenyeviti, lakini kama mihuri inaweza kupunguza heshima yenu nimeona kufuta muongozo huu Mpaka pale tutakapo jadili tene upya swala hili" amesema

Sanjari na hayo Waziri Simbachawene amefafanua kuwa kulikuwa na sababu za msingi za kutoa muongozo huo wa kutokutumia mihuri kutokana na matumizi mabaya ya mihuri kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa na kupelekea kuigawa ardhi bila utaratibu maalumu.

Hata hivyo Katibu wa Wenyeviti Mkoa wa Dar es salaam Mariam Machicha ameishukuru Serikali kwa kuona tatizo hilo na kuahidi kulifanyioa kazi.


Share:

Kilichotokea Hadi Kupelekea Kukamatwa Kwa Edward Lowassa

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, limemkamata Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Lowassa ambaye pia alikuwa mgombea urais wakati wa uchaguzi mkuu mwaka juzi kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amekamatwa mjini Geita jana muda mfupi baada ya kuwasili akitokea Mkoa wa Kagera alikokuwa kwa shughuli za kisiasa.

Mbali na Lowassa, viongozi wengine waliokamatwa ni Profesa Mwesigwa Baregu na Hamis Mgeja.

Lowassa na wenzake hao, walikuwa wakielekea Kata ya Nkome, Jimbo la Geita Vijijini kushiriki mkutano wa kampeni za udiwani.

Tukio hilo lilitokea jana saa 9:20 mchana baada mwanasiasa huyo kuwasili mjini Geita na kukuta wananchi wengi wakiwa wamejaa barabarani wakitaka awasalimie.

Kutokana na umati mkubwa wa watu waliokuwa barabarani, Lowassa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, yeye na msafara wake walilazimika kuingia eneo la stendi ya zamani ya mabasi kuwasalimia wananchi hao.

Hata hivyo, kabla hajaanza kuzungumza na wananchi hao, magari matatu yaliyokuwa yamejaa askari polisi yalifika mahali hapo na kumkamata.

Baada ya kufikishwa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita na kukaa kwa dakika kadhaa, Lowassa na wenzake walihamishiwa ofisini kwa Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo kwa mahojiano.

 MABOMU YA MACHOZI

Baada ya mwanasiasa huyo kukamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita, kundi la wananchi wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema, walianza kueleka maeneo ya kituo hicho ili kujua kinachoendelea.

Wakati wakielekea katika eneo hilo, polisi walilazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi yaliyoathiri wanafunzi wa Shule ya Msingi Mseto.

 WAANDISHI WAPIGWA

Wakati hayo yakiendelea, baadhi ya waandishi wa habari walijikuta wakiwa katika wakati mgumu wa kufanya kazi zao baada ya kukamatwa na kupigwa na polisi.

Miongoni mwa waliopigwa ni Mwandishi wa Habari wa Chanel Ten, Vales Robert na Joel Maduka wa Stom Radio.

Akizungumzia tukio hilo, Robert alisema yeye na mwenzake walipigwa baada ya kushutumiwa na polisi, kwamba walikuwa wakipiga picha za tukio la Lowassa kukamatwa.

“Tulivamiwa na polisi wakati tukipiga picha na wakati tunapigwa, tulikuwa tumevaa vitambulisho vyetu vya uandishi wa habari.

“Yaani wamenivunjia kamera yangu, lakini nashukuru sijaumia sana,” alisema Robert.

 KAMANDA WA POLISI

Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Geita, Mwabulambo, alipopigiwa simu kuhusu suala hilo, simu yake ilipokewa na msaidizi wake ambaye alisema alikuwa katika kikao na Lowassa.

“Mimi ni mlinzi wa afande RPC, samahani yupo kwenye kikao na mheshimiwa Lowassa, nakuomba umtafute baadaye,” alisema bila kutaja jina lake.

Kutokana na tukio hilo, viongozi mbalimbali wa Chadema Mkoa wa Geita, walikuwa katika ofisi za Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Geita ili kujua hatma ya tukio hilo.

Kukamatwa kwa Lowassa na wenzake hao ni mwendelezo wa viongozi wa Chadema kukamatwa baada ya Januari 14, mwaka huu, Jeshi la Polisi, Mkoa wa Geita kumkamata Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Geita, Upendo Peneza.

Mbunge huyo baada ya kukamatwa, aliunganishwa kwenye kesi ya uchochezi na Diwani wa Kata ya Kasamwa, Fabian Mahenge wakituhumiwa kufanya uchochezi huo Januari 6, mwaka huu katika mkutano wa hadhara.

Kabla ya kumkamata Peneza, polisi waliwakamata Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Bara), John Mnyika na Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Kagera, Conchesta Rwamlaza, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Geita, Anna Rose.


Share:

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger