May 8, 2016

Mwarobaini Migogoro ya Ardhi Wapatikana..Hati Miliki za Kimila Kuanza Kutolewa

Malinyi Baada ya kukithiri kwa migogoro ya ardhi katika vijiji vingi hapa nchini, serikali kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi wameamua rasmi kutafuta mwarobaini wa kuondoa changamoto hiyo kwa kuanzisha mpango maalumu wa utoaji wa Hati Miliki za Kimila kwa kila ardhi ndani ya vijiji vyote nchini.

Mkurugenzi wa Mipango Miji na Vijiji kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa John Lupala amesema mpango huo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka kumi kupitia mafunzo watakayoyapata kupitia mradi wa kuanzisha programu kuwezesha Umilikishaji Ardhi(LTSP).

Profesa Lupala alitoa kauli hiyo jana wilayani Malinyi dakika chache kabla ya kuanza kwa mkutano ulioshirikisha madiwani, maofisa ardhi, mipango miji, maofisa wa hifadhi na watendaji wa serikali kwa lengo la kuchambua na kuingiza maoni mapya katika rasimu ya kwanza ya mpango wa matumizi bora ya ardhi katika wilaya hiyo.

Hatua hiyo ni sehemu ya ziara ya siku nne ya watalaamu watakaotekeleza Hatimiliki za Kimila kwa wanakijiji zaidi ya 300,000 kwa wilaya ya Kilombero, Ulanga na Malinyi kupitia mradi huo.

Kwa mujibu wa mradi huo wenye thamani ya dola 15.2milioni kupitia hisani ya nchi za Swideni, Denmark na Uingereza,umelenga ardhi na kugawa hatia hizo kuanzia mwaka huu hadi ukomo wake 2019.

Alisema utekelezaji huo utategemea zaidi kushirikisha sekta binafsi. Alisema njia zinazotumika katika utekezaji wa mradi huo zitasaidia katika kurahisisha mpango wa miaka miaka kumi kwa vijiji vingine vyote nchini.

“Kwa sasa nchi nzima ina vijiji takribani 12,000 na vijiji wastani wa 9000 vimeshapimwa mipaka yake lakini changamoto iliyopo ni kwamba, kuna vijijiji 1640 tu vilivyopangiwa matumizi ya ardhi, utaona bado safari ni ndefu,kwa hivyo mbali na mradi wa LTSP, kuna programu hiyo inakuja bado iko kwenye maandalizi,” alisema.

Akizungumzia hali ya migogoro na hatua za utekelezaji wa mradi huo, Profesa Lupala alisema uwazi ndiyo utakaofanikisha kukamilisha ugawaji wa hati hizo na itakuwa fundisho kwa hatua nyingine za kusaidia wananchi ili ardhi wanayoitumia iwanufaishe kiuchumi.

Kwa upande wake, Mwanasheria wa wilaya hiyo ya Malinyi, Beatrice Buya alisema asilimia 100 ya kesi anazopokea ofisini kwake ni migogoro ya ardhi. Alisema mbali na mradi huo wa LTSP, Julai  mwaka huu wilaya hiyo inatarajia kuanza utekelezaji wa mpango mpya wa matumizi bora ya ardhi ili kupunguza migogoro.

Isaya Mwilongo ambaye ni mkazi wa kijiji cha Makelele, wilayani hapo alisema chanzo cha migogoro hiyo ni mchezo mchafu wa viongozi wa serikali za vijiji na kamati za ardhi kumilikisha ardhi kubwa kundi la watu wachache.

“Mimi ni mmoja kati ya waathirika na leo nilikuja kuonana na wataalamu waniambie kwanini ardhi yangu ya kijiji cha Kihuvilile(hekari 4), sijapewa na mahamaka ya Ulanga na Kilombero zimeshaamua mwaka 2012 nikabidhiwe lakini kuna ujanja ujanja wa kutapeliwa kwa nguvu,”alisema.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger