May 9, 2016

Taasisi ya Saratani Ocean Road ni Mateso

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) imepewa asilimia 0.3 tu ya dawa ilizoomba wizarani kwa mwaka 2015/16, hali inayosababisha mateso kwa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo.

Akizungumza na Mwananchi wiki iliyopita, Meneja Famasia wa ORCI, Albina Kirango alisema dawa hizo zimekuwa zikifikishwa hospitalini hapo kwa mafungu na kuanzia Julai hadi Septemba walipokea asilimia 0.02, Oktoba mpaka Desemba asilimia 0.05 huku Januari mpaka Machi wakipokea asilimia 0.2.

Kirango alisema Ocean Road huagiza dawa kupitia Wizara ya Afya, kwa kuorodhesha idadi ya dawa wanazozihitaji na kuwasilisha Bohari Kuu ya Dawa (MSD), huku nakala nyingine ikipelekwa wizarani ambako hutolewa fedha kwa ajili ya kuzilipia.

“Tunaweza kuagiza aina 15 za dawa za saratani, lakini iwapo wizara ikatoa kiasi kidogo cha fedha huletwa dawa zenye umuhimu, lakini za gharama ya chini ili angalau kuhudumia wagonjwa wengi zaidi, maana zipo dawa ambazo gharama yake ni Sh3 milioni mpaka 4 milioni kwa dozi ya wiki mbili,” alisema Kirango.

Kiwango hicho cha dawa kilitolewa kulingana na kiasi cha fedha ambacho kimekuwa kikitolewa na Wizara ya Afya, kama bajeti ya matumizi ya taasisi hiyo inayohudumia zaidi ya wagonjwa 6,000 kila mwaka.

Alisema dawa hizo za tiba ya saratani kwa kemikali ‘Chemotherapy’ zimekuwa zikiadimika zaidi hospitalini hapo, hivyo kuwafanya baadhi ya wagonjwa kulazimika kuzinunua nje ya hospitali katika maduka mbalimbali ya dawa.


  • “Katika dawa zote tunazoagiza, tumekuwa tukiletewa idadi pungufu, lakini dawa hizi zinapatikana kwa shida ukizingatia gharama zake kuwa kubwa,” alisema Kirango.


Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alipoulizwa alisema mbali na bajeti ya 2015/16, wizara ina mpango wa kuhakikisha tatizo hilo linatokomezwa na wagonjwa wanapata dawa.

“Wizara kuanzia Januari mwaka huu wizara ilianza kutenga asilimia 13 ya bajeti ya dawa kila mwezi, kwa ajili ya dawa hizo na hadi sasa wizara imepeleka MSD Sh1.2 bilioni kwa ajili ya kununua dawa hizo na bohari hiyo inafanya utaratibu wa kuzinunua kwa wazalishaji hivyo tatizo hili litapungua,” alisema Ummy Mwalimu.

Kwa mujibu wa Kirango, dawa ambazo zimekuwa zikipelekwa mara chache hospitalini hapo ni pamoja na Doxorubicine, Cyclophamide na 5FU ambazo hutibu saratani ya titi.

“Kuna baadhi ya dawa kama ‘Cyclophamide’ tuna zaidi ya miaka minne hatujaletewa, Bevazicumas hii gharama yake ni Sh1.8 milioni, Rituximab Sh4.23 milioni, Transtuzuma Sh3.7 milioni na mgonjwa anatakiwa kupewa kila baada ya wiki mbili kwa kuwekewa kwa dozi sita,” alisema Kirango.

Mkurugenzi wa Tiba wa Ocean Road, Dk Diwani Msemo alisema licha ya uhaba wa dawa hospitalini hapo, asilimia 80 ya wagonjwa wanaotibiwa hapo wanatumia tiba ya mionzi ambayo matibabu yake ni bure.

Alisema tatizo ni kuwa baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakitumia dozi zote mbili yaani radiotherapy na chemotherapy kwa wakati mmoja, huku wengine wakitumia mojawapo kati ya hizo.

“Tunashukuru bajeti mwaka huu imependekeza kutengwa kwa Sh9 bilioni kwa ajili ya dawa, hii itasaidia kwa wagonjwa ambao wanashindwa kumudu gharama, kwani wagonjwa pia wamekuwa wakiongezeka kila mwaka,” alisema Dk Msemo.

Dk Msemo alisema wagonjwa wengi ni maskini, hivyo inakuwa vigumu kumudu matibabu na kusababisha wengine kurudi nyumbani kwa kukosa fedha kutokana na gharama iliyopo.

“Matibabu ya saratani ni ghali, lakini Serikali ya Tanzania imekuwa ikitibia bure wakati mwingine mgonjwa anapofika anatakiwa kutibiwa kwa mionzi pekee, lakini tiba ya kemikali ni gharama,” alisema.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger