Jun 28, 2016

Jukwaa huru la wazalendo latoa neno kuhusu teuzi za Wakuu wa Wilaya wapya

JUKWAA HURU LA WAZALENDO TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

VIONGOZI WATEULE TUKACHAPE KAZI KWELI KWELI​

Ndugu waandishi wa habari salaam!
Poleni na majukumu ya kila siku ya ujenzi wa Taifa.
Leo Jukwaa Huru La Wazalendo Tanzania, tumewaiteni hapa kueleza na kupongeza jitihada za mh John Joseph Pombe Magufuli rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuwaletea wananchi maendeleo yao wenyewe.

Ndugu wana habari, JuhWaTa linatumia fursa hii kwanza kabisa, kumpongeza mh rais kwa teuzi za wakuu wa wilaya alizofanya hivi karibuni. Mh rais amezidi kudhihirisha kuwa yeye ni kiongozi anayeishi na kusimamia kile anachoahidi kwa vitendo, mh rais alisema nanukuu "... _Nimeona vijana ndio wachapakazi, wasiopenda rushwa na Wazalendo, hivyo nitaendelea kuwaamini ndani ya serikali yangu kwa kuwateua kunisaidia kazi mbalimbali_ ..." mwisho wa kunukuu na hili amelitimiza na kulithibitisha katika teuzi hizi za wakuu wa wilaya ambapo kwa zaidi ya 70% ya wateuliwa wote ni vijana. Sote tunajua vijana wana ari, utayari na shauku ya kuongoza kwa sifa za kiuongozi ambazo ni Uadilifu, Ubunifu, Uwajibikaji na Uzalendo. Hongera sana mh rais.

Ndugu wana habari, Jukwaa limefurahishwa kwa kitendo cha mh rais JP Magufuli kwa kuzidi kujipambanua zaidi na zaidi kuwa yeye ni rais wa Watanzania wote pasipo kujali itikadi zao husasan za kisiasa. Teuzi hizi zimesadifu taswira nzima ya mh rais kwani amezingatia zaidi Uadilifu, Uwajibikaji, Uzalendo na uwezo wa kiongozi husika katika kuunganisha wananchi ili kufikia maendeleo yao wenyewe na Taifa kwa ujumla kuelekea kuwa nchi ya Uchumi wa kipato cha kati. Tunampongeza sana.

Ndugu wana habari, Jukwaa pia linawapongeza wateule wote kwa kupewa heshima kuu na imani ya pekee kutoka kwa mh rais pia tunatoa Rai kwa Wateule wote ya kuendelea kujitathmini na kujiuliza mara mbili mbili ni vigezo gani mh rais ametumia kuwaamini wao na sio wale? Ni imani ipi rais amewapa wao na sio hawa wengine? Nawashauri wakafuate hatua na kuendelea kumjengea mh rais imani juu ya vijana vile walivyofanya vijana wenzao waliotangulia katika nafasi mbalimbali za Ukuu wa Mikoa, Ukatibu mkuu, Uwaziri, unaibu waziri, Ukuu wa Wilaya nk iliyopelekea kufungua milango kwa vijana wengi zaidi. Kachapeni kazi njema mzidi kufungua milango mingi zaidi kwa vijana wengine.
Jukwaa limejiridhisha kuwa mh rais ni kiongozi asiyependa kutenda kwa mazoea, Mazoea ni kujisahau. Tukachape kazi kweli kweli ya kumsadia mh rais katika adhma yake ya dhati ya kuwatumikia Watanzania wote bila kujali rangi zao, dini zao, sehemu zao na vyama vyao. Maendeleo ni ya Watanzania wote na Taifa kwa ujumla.

Kwa kuhitimisha Jukwaa linatoa Rai kwa Watanzania wote, viongozi wote wa dini na kisiasa tuendelee kumuunga mkono mh rais katika harakati zake za kutuletea maendeleo Watanzania wote.
Pia Tunawatakia ndugu zetu Waislam wote mfungo katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan. Na kila la kheri timu ya Yanga African wawe na mchezo wa ushindi dhidi ya timu ya TP Mazembe ya DR Congo.
Ahsanteni sana.

*Imetolewa* _28/06/2016_ DSM.
Mtela Mwampamba.
Katibu Jukwaa Huru La Wazalendo Tz. 0755178928

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger