Jun 28, 2016

Wakuu wa Wilaya Wapya, Muwe Tochi ya Maendeleo

KWANZA nianze kumuomba Mungu azidi kutupa afya njema ili tuweze kumtumikia vema na kutumikia taifa letu huku tukidumisha amani yetu.

Leo nizungumze na wakuu wa wilaya wapya walioteuliwa na Rais Dk. John Pombe Peter Magufuli juzi Jumapili ambao hakika ndiyo viongozi walio karibu zaidi na wananchi wa chini kabisa. Nasema hivyo kwa sababu mkuu wa wilaya ndiye anayeshughulika na serikali za vijiji au mitaa moja kwa moja na ndiye anayekutana mara nyingi na wananchi hao kujadili mambo mbalimbali ya maendeleo katika ngazi hizo za chini za uongozi.

Bila shaka watajulishwa majukumu yao lakini ni wazi kwamba watatakiwa wasishinde ofisini badala yake wawe kwenye vijiji au mitaa kusikiliza kero za wananchi na kuzifanyia kazi.
Mkuu wa wilaya ndiye mwakilishi wa rais katika ngazi ya wilaya na ndiye ana majukumu ya kuhakikisha usalama katika wilaya yake ndiyo maana anakuwa moja kwa moja mwenyekiti wa kamati ya usalama ya wilaya.

Ni jukumu la kila mkuu wa wilaya kuhakikisha wilaya yake haina wavurugaji wa amani ambao ni pamoja na majambazi na watu wanaoua watu kwa njia mbalimbali.
Niwaambie ukweli wakuu wa wilaya wapya kwamba ili mfanikiwe ni lazima muwe karibu na wananchi wa kawaida kwa sababu hao ndiyo wanaokaa na watu, wawe wema au wabaya.
Kila mkuu wa wilaya ni lazima awe pia karibu na wana habari kwa sababu hao hujikita zaidi na wananchi mitaani ndiyo maana wanapata habari wakati mwingine nyeti za kusaidia amani na utulivu nchini.

Niwasihi wakuu wa wilaya kuepuka ushabiki wa kisiasa. Wapo ambao wanapendelea mara kwa mara kujikita katika siasa wakati wanajua wao wanahudumia watu wa vyama vyote. Mkuu wa wilaya kujiingiza katika siasa za moja kwa moja ni kosa kwa sababu watu wa upande wa pili wanaweza kuwatenga.

Nasema hivyo kwa sababu kuna wilaya zimekamatwa na wapinzani kwa maana ya halmashauri ya wilaya inaongozwa na wenyeviti wapinzani ni jukumu la mkuu wa wilaya kufanya kazi vizuri ili wilaya hizo nazo zipate maendeleo kwa sababu wanaohudumiwa siyo vyama bali ni wananchi.
Nasema ni wananchi kwa sababu upo ushahidi kwamba katika wilaya nyingine kuna wananchi ambao siyo wanachama wa vyama vya siasa ndiyo maana katika katiba pendekezwa ikapendekezwa kuwa wasio wanachama wa vyama vya siasa nao waruhusiwe kupigiwa kura.

Kwa maana hiyo niwasihi wakuu wa wilaya wapya kuacha kuegemea chama licha ya kujua kwamba wameteuliwa na kiongozi ambaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi.
Maana yangu ni kwamba shughuli za chama zisihusishe moja kwa moja na shughuli za maendeleo kwa kuwa kwa kufanya hivyo, mtapoteza watu wa upande wa pili hivyo kukosa kile kilichokusudiwa.

Mwisho, nimpongeze Rais Dk. Magufuli kwa hatua yake ya kuchagua vijana wasomi kutuongozea wilaya zetu tukiwa na imani kuwa watachapa kazi kama alivyoonesha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye haraka haraka amepanda na kuwa mkuu wa mkoa kutoka wilayani. Huyu anaweza kuwa tochi yenu nanyi mkawa tochi ya wananchi. Atakayekwenda kwa kuchechemea, ataachwa nyuma!

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger