Jul 1, 2016

Mahakama ya Mafisadi Kuanza Rasmi Leo

MAHAKAMA Maalumu ya kushughulikia Makosa ya Rushwa na Ufisadi, inaanza rasmi leo Julai mosi.

Pamoja na kuanza kwa mahakama hiyo, serikali imeanza mchakato kuifanyia marekebisho Sheria Namba 11 ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini ya Mwaka 2007 ili kuongeza ukubwa wa adhabu zinazotolewa sasa.

Mahakama hiyo iliyoahidiwa na Rais John Magufuli wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na imo katika Ilani ya Uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi, itaimarisha zaidi taasisi za uwajibikaji zinazohusika na mapambano dhidi ya rushwa.

Ahadi hiyo ambayo inatimizwa ndani ya kipindi cha miezi isiyozidi saba tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani ni sehemu ya mapambano ya kujenga misingi ya uchumi kwa kudhibiti rushwa na mianya yake na kuleta uwajibikaji.

Akiahirisha Bunge jana mjini Dodoma, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alisema utekelezaji wa ahadi hiyo unakwenda sambamba na kuonesha dhamira ya serikali ya kushughulikia makosa ya rushwa na kuweka misingi imara ya uwajibikaji katika sekta zote.

“Mahakama itawafanya watu waliozoea rushwa na ufisadi kujiuliza mara mbili kabla ya kufanya uhalifu huo yaani kuwa deterrent,” alisema Waziri Mkuu na kuongeza kuwa kuwapo kwake kutahamasisha wafanyabiashara kufanya shughuli zao bila shaka huku umuhimu kwao, ikiwa ni kulipa kodi.

Akielezea umuhimu wa mahakama hiyo, alisema kwamba itasaidia kuendeleza nia ya serikali ya watu kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa.

Akielezea umuhimu wa kodi, alisema kuna mahitaji makubwa ya fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na uendeshaji wa shughuli za serikali na hivyo serikali itaendelea ukusanyaji wa mapato ya ndani na kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi.

Aidha, alisema serikali itaanzisha Kikosi Maalumu cha kufuatilia kwa karibu matumizi ya mashine za kielektroniki (EFDs) za kutoa risiti kila mfanyabiashara anapouza bidhaa au huduma na kuhakikisha kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) wanashirikiana na Wakala wa Serikali wa Serikali Mtandao kutekeleza mfumo wa kuwa na dirisha moja na pia kudhibiti kikamilifu mizigo inayoingia na kutoka bandari kavu.

Udhibiti wa matumizi
Akizungumzia matumizi, Waziri Mkuu alisema serikali itaendelea na kudhibiti matumizi yasiyokuwa ya lazima na kufuatilia bajeti na matumizi ya fedha za umma.

Na ili kufanikisha hilo, itafanya mapitio ya majukumu ya wizara na taasisi za umma ili kuwianisha majukumu ya vyombo vya serikali na hivyo kupunguza gharama za uendeshaji.

Aidha, uhakiki wa wafanyakazi utaendelea na watendaji wakitakiwa wanadhibiti matumizi ya fedha za umma kwa kuzingatia ukomo wa bajeti ya fungu husika lililoidhinishwa na Bunge.

Aidha, Waziri Mkuu aliagiza halmashauri zote nchini kuanzia leo kuhakikisha kwamba zinatumia mifumo ya kielektroniki katika kukusanya mapato, kulipa, kuweka na kutekeleza kikamilifu mikakati madhubuti ya kuboresha makusanyo iwe yanafanywa na halmashauri au kupitia wakala wake.

Waziri Mkuu alisema wabunge wamepitisha Bajeti ya Serikali inayotegemea sana ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kupunguza utegemezi kutoka nje na kuhimiza uwajibikaji katika kuongeza juhudi za kukusanya na kupanua wigo wa kutoza kodi ili mapato yaongezeke.

Aidha, alisema ipo haja ya wananchi kudai risiti kwa huduma mbalimbali wanazonunua na kushirikiana na serikali kubaini wakwepa kodi na kuziba mianya ya upotevu wa mapato ya serikali.

Aliwataka watumishi wa umma kuendelea kufanya kazi kwa maadili katika maeneo yao wakijenga utamaduni wa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika utumishi wa umma ili kuongeza ufanisi na tija.

Mpango wa Maendeleo
Akizungumzia maeneo manne ya Mpango wa Maendeleo, Waziri Mkuu alisema kwa sasa Serikali ya Awamu ya Tano imeweka msingi kupitia Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa kukuza na kujenga uchumi wa viwanda kwa kuweka mazingira yatakayochochea maendeleo ya viwanda.

Aidha, imejiweka katika hali ya kufungamanisha maendeleo ya uchumi na maendeleo ya watu kwa kuhakikisha kwamba elimu inayotolewa ni bora na inayojenga msingi wa rasilimali watu wanaohitajika kuipeleka nchi katika uchumi wa kati.

Alisema ili kufanikisha hayo serikali itaimarisha mifumo ya kisheria kuwa rafiki na kuvutia wawekezaji wa ndani na nje huku ikiimarisha miundombinu ili iweze kutumika kirahisi na kupunguza gharama zake.

Ili kufanikisha ufanisi na tija, Waziri Mkuu alisema serikali itaimarisha usimamizi, ufuatiliaji na tathmini ya mpango wenyewe wa maendeleo mara kwa mara.

Ili kufanikiwa ametaka tabia ya vijana kushinda katika pombe na kucheza pool table kuachwa na kuwataka viongozi waliochaguliwa sasa wilayani na mikoani kuhakikisha kwamba maeneo ya starehe hayafunguliwi wakati wa muda wa kazi ili vijana washiriki katika uzalishaji mali.

Akizungumzia mkakati wa ujenzi wa uchumi wa viwanda, Waziri Mkuu alisema serikali itategemea zaidi sekta binafsi kama injini ya ukuzaji uchumi na maendeleo na kwamba serikali haitajiingiza moja kwa moja katika kujenga viwanda na kufanya biashara.

Miradi ya umeme
Akizungumzia uimarishaji wa uchumi kwa kuwa na uhakika wa nichati hadi vijijini, alisema serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuyapatia maeneo yaliyo nje ya gridi ya taifa nishati bora ikiwa ni pamoja na maeneo ya visiwani.

Alisema Serikali ya Uingereza na Sweden zinachangia katika kuhakikisha kwamba mifumo hiyo ya kupeleka umeme maeneo yaliyo nje ya gridi inafanikiwa. Alisema serikali imetenga zaidi ya Sh trilioni moja kutoka ndani na benki ya dunia kwa ajili ya kuendeleza nishati vijijini.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger