Sep 13, 2016

Utendaji Makini wa Mh Rais Magufuli Wapaisha Sekta ya Utalii


Utendaji wa JPM waipaisha sekta ya utalii Uchambuzi wa kina wa hali ya mambo katika sekta moja muhimu ya utalii, eneo linaloiingizia Serikali takribani asilimia 25 ya fedha za kigeni, unaonesha, pamoja na kelele za hivi karibuni, watalii wengi wameongezeka nchini hasa katika kipindi cha Julai mpaka Agosti mwaka huu ikiwa ni ongezeko la asilimia 11.

Uchunguzi zaidi umeonesha kuwa watalii wengi waliokuja nchini au wanaofikiria kuja nchini hawajaguswa na ongezeko hilo la kodi zaidi ya kujali aina ya vivutio vilivyoko nchini, hali ya amani na wapo wanaovutiwa pia na utawala wa Rais John Pombe Magufuli ambaye anasikika duniani kote hivyo wanakuja kuona hali ya siasa nchini.

Katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, takwimu za watalii waliotembelea hifadhi hiyo, kwa kipindi cha Juni hadi Agosti, 2015 na Juni hadi Agosti, 2016 nako zinaonesha ongezeko. 

“Kwa kulinganisha idadi ya watalii waliotembelea Hifadhi ya Ngorongoro kwa miezi mitatu (Juni-Agosti 2015) na mwaka Juni hadi Agosti,2016, inaonekana kuwa idadi ya wageni imeendelea kuongezeka hivyo mapato pia yameongeza. 

“Kwa mantiki hiyo hadi sasa utekelezaji wa kodi mpya haujaathiri mapato na haijawa kikwazo bado kwa watalii kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro,” inasema taarifa ya hali ya utalii nchini ambayo gazeti hili limeiona sehemu yake.

Tayari watalii wenyewe na wataalamu wa sekta hiyo waliokuja nchini kwa wingi licha ya kodi kuongezeka, ripoti hiyo ya kina inaainisha, wengi hawakuonekana kubabainishwa na kodi hiyo:

“Watalii waliohojiwa kwenye malango na mahoteli walionyesha kutoelewa kuwa VAT imeanza kutozwa na baadhi walishangaa kwamba Serikali haikuwa inatoza kodi fedha zilizokuwa zinalipwa na watalii waingiapo Hifadhini,” inasema ripoti hiyo. 

Akiandika katika makala yake iliyoandikwa kwa lugha ya kiingereza Why VAT will not kill hotels, tourism na kuchapishwa na gazeti moja la kila siku nchini, mmoja wa walimu wanaofanyakazi nchini Australia na mtalii wa mara kwa mara kuja Tanzania na sehemu nyinginezo Afrika, Sabine Barbara anasema:

“Hali ya kisiasa ya nchi inaweza kuwa na athari zaidi kwa watalii kuliko kuongezeka kwa ada za kuingia katika mbuga za wanyama….juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano zitapimwa unapofika mwisho wa mwaka kuliko kuanza kuwatisha watu hivi sasa kuwa kodi zitapunguza watalii.”

Takwimu hizi zinakuja wakati ambapo wiki iliyopita akizungumza katika kipindi cha TUNATEKELEZA, kinachorushwa na TBC1, Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akidokeza na kuthibitisha kuwa kodi mpya ya VAT haikuwa imeathiri idadi ya watalii wala mapato ya nchi.

Akizungumzia jana na gazeti hili kuhusu kuongezeka kwa watalii licha ya wasiwasi wa awali wa kodi hiyo ya VAT, Meneja Mawasiliano wa TANAPA, Bw. Paschal Shelutete, alisema ni kweli kuna ongezeko hilo na wao walilitarajia.

“Ni kweli kwamba watalii wameongezeka kuja kutembelea hifadhi zetu na vivutio vingine vya nchi. Hakuna mtalii anayeweza kushindwa kuja nchini kwa sababu ya kutakiwa kulipa kodi. Bahati nzuri wenzetu wanautamaduni wa kuheshimu sana kodi na ndio maana hawajastushwa na kodi hiyo,” alisema.

Takwimu hizi, hasa katika kuelekea mwaka mmoja wa uongozi wake, zinampa Rais Magufuli nguvu ya kuendeleza zaidi utawala wake unaojikita katika kuhakikisha kodi za Serikali zinalipwa ili kuiongezea Serikali mapato kwa lengo la kufikia azma ya kujitegemea.

Itakumbukwa kuwa Julai mwaka huu Serikali ilianza kutekeleza kodi mpya ya ongezeko la thamani (VAT) katika sekta ya utalii, hatua iliyopingwa na wadau wa sekta hiyo kuwa ingeathiri idadi ya watalii wanaokuja nchini.

Miezi miwili baadaye, takwimu zinathibitisha kuwa ongezeko hilo la kodi ambalo Rais Magufuli mwenyewe amepata kulitetea, tofauti na mawazo ya wengi, halijaathiri, na badala yake sababu nyingine kama vivutio vilivyopo nchini na hali ya amani na utulivu vimeendelea kuifanya Tanzania iwe na mvuto zaidi kwa watalii.

Takwimu ambazo kutoka kutoka vyanzo mbalimbali Serikalini, sekta binafsi na kwa wadau wa utalii wenyewe, zinathibitisha kuwa wakati kwa mwaka mzima wa 2015 idadi ya watalii waliongia nchini ilikuwa 1,1376,182 idadi hiyo imeongezeka mwaka huu.

Takwimu hizo zinaonesha kuwa kwa kuangalia ulinganifu wa takwimu za mwaka jana kipindi kama hiki na mwaka huu, takwimu za Hifadhi za Taifa (TANAPA), zinaonesha idadi ya watalii wote katika kipindi cha Juni-Julai 2016 imeongezeka kwa sana.

Ongezeko hilo pia limeongeza mapato yatokananyo na viingilio hifadhini ambapo yameongezeka kwa wastani wa asilimia 19.7 huku mapato yatokanayo na vyanzo vingine yakiongezeka kwa wastani wa asilimia 13.

Julai mwaka huu, Serikali ilianzisha kodi ya VAT ambayo itakuwa ikikatwa kwenye huduma za uongozaji watalii, kuvinjari (safari) na ada za viingilio (park fees) hifadhini. Huduma za malazi zilishakuwa zikitozwa kodi hiyo tangu awali.

“Baada ya miaka ya 10 sekta ya utalii kufaidika na msamaha huo, Serikali iliona sekta imeimarika na ni vema sasa ichangie zaidi katika mapato ya nchi moja kwa moja kwa kuondoa msamaha huo,” anasema mtaalamu mmoja wa masuala ya kodi katika sekta binafsi na kuongeza:

“Hivyo, msamaha huo ulifutwa kupitia Finance Act ya mwaka 2016 (Juni). Takwimu am,bazo hata sisi tunazo zinaonesha katika kipindi hiki cha Julai na Agosti, 2016 ambapo huduma za utalii zimeanza kutozwa VAT hapakuwa na athari ya mapato kwa Serikali.”

Na Mwandishi Wetu, Gazeti la Majira, Sept., 13, 2016 

WAKATI Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli ikielekea kutimiza mwaka mmoja Novemba mwaka huu, mageuzi makubwa anayoyafanya, staili yake binafsi ya uongozi na mafanikio katika kulinda misingi ya amani vimeendelea kuwavutia wageni wengi duniani.

Katika kuelekea mwaka mmoja wa Serikali ya Magufuli, wachambuzi wanaweza kutazama utawala wake kwa namna tofauti kwa kuangalia na kuzingatia nyanja za uchumi, siasa, jamii na teknolojia.
Uchunguzi wa unaonesha kuwa sera na staili ya uongozi wa Rais Magufuli hasa katika nyanja za uchumi zimeanza si tu kuwavutia wageni kutoka nje lakini pia kuipatia nchi mapato yaliyokuwa yakipotea awali.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger