Oct 20, 2016

Ali Kiba, Sallam Wametoka Mbali

Wiki mbili zilizopita, Ali Kiba alikuwa mmoja kati ya mastaa wa muziki waliopafomu kwenye Tamasha la Rock lililofanyika Viwanja vya Golf, Mombasa.

Katika tamasha hilo lililokuwa na staa kutoka Marekani, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ na Ayodeji Balogun ‘Wizkid’ kutoka Nigeria liligeuka kuwa na sintofahamu baada ya Ali Kiba kupanda na kupafomu nyimbo mbili tu, ikiwemo Mac Muga kisha kuzimiwa kipaza sauti.
Malalamiko ya Ali Kiba (pichani juu) juu ya tukio hilo aliyaelekeza moja kwa moja kwa meneja wa Diamond Platinumz, Sallam Sharaff ambapo alisema;

“Mkataba waliokubaliwa ulikuwa Chris Brown apafomu kwa dakika 80 na pale muda ulikuwa umekwenda sasa sijajua kitu gani kimefanyika mpaka imekuwa hivyo. Kuna vitu sikuvielewa yaani sikufurahishwa navyo, nilimuona meneja wake Diamond, Sallam. Yeye alifuata nini backstage. Japo watu wanafikiria sina bifu na Diamond, sasa yeye alikuwa kafuata nini? Kuna watu wengi walikuja kwenye shoo na kuna hadi VIP, yeye alifuata nini backstage?”

Alichojibu Sallam, alikuwepo hapo kwa sababu ya ukaribu na Meneja wa Wizkid, Sunday.
“Meneja anayesimamia kazi (connection) za Diamond Afrika Magharibi ni Mr Sunday. Kwa Afrika Mashariki anayesimamia kazi za Wizkid ni mimi. Kuja hapa (Mombasa) ni kitu cha kawaida kabisa. Wakati anapafomu mi sikuwepo kabisa eneo lile.

“Tushirikiane, tuache kujenga chuki, kama niliwakwaza watu wote wa Kenya na walinichukulia kama nilimfanyia nia mbaya Ali Kiba wanisamehe. Naomba na yeye Kiba awaombe msamaha mashabiki wote wa Kenya. Nachosema pole Kiba, shoo yako haikuwa nzuri, ukaona lawama umpe f’lan.”

Ingawa kumekuwa na madai ya kuwepo kwa bifu kati ya mastaa wawili, Diamond na Ali Kiba, wote wawili kwa nyakati tofauti wamekuwa wakikanusha. Kuna timu zimeundwa, kuna wadau wamegawanyika, lakini wenyewe kila mara wanasema no bifu kati yao.
Hata hivyo, yapo baadhi ya matukio yanayoonyesha chembechembe za ukweli juu ya sintofahamu baina ya mastaa hao wawili. Lakini kwa umakini, kinachoendelea kati ya Sallam, mtu anayetajwa kuwa nyuma ya mafanikio ya Diamond na Ali Kiba, siyo kitu cha kubeza, kwani ‘mvutano’ baina yao unaanzia mbali.


Januari, 2015
Katika shoo iliyofanyika Januari 2015, Viwanja vya Leaders jijini Dar ambayo iliandaliwa na Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo ikitambulika kama Tigo Kiboko Yao, mastaa mbalimbali wa Bongo Fleva walialikwa kutumbuiza akiwemo Diamond na Ali Kiba.
Kiba hakutumia mlango maalum wa VIP kuingia ndani, bali kwa sababu anazozijua mwenyewe aliruka ukuta na kuingia backstage. Alipotua, watu wa karibu kabisa walikuwa ni MwanaFA na Shaa ambao kwa anachojua mwenyewe pia, akawakaushia, akapitiliza moja kwa moja jukwaani na kuanza amsha-amsha.
Ni usiku huohuo ambao Diamond alizomewa na kurushiwa chupa za maji na mashabiki. Pengine kwa kujua namna ya kuwatuliza, mkali huyo wa kibao cha Kidogo, aliwarushia noti za shilingi elfu mbilimbili, akafanikiwa kuwanyamazisha mazima.
Kesho yake, Sallam kupitia ukurasa wake wa Twitter aliandika maneno yaliyoonyesha kumlenga King Kiba;
“Umeruka ukuta, wametupa chupa, zikawaishia, umemzuia @mwanaFA @Shaa_tz wasikusalimie, uliowalipa wakarushiwa buku mbilimbili WAKAKUSALITI.”

Agosti, 2015 
Katika msimu wa tatu unaowashirikisha wasanii wa mataifa mbalimbali kujumuika pamoja na kufanya kolabo ya nyimbo zao, Coke Studio ilimualika Ne-Yo pamoja na wasanii kutoka Afrika wakiwemo Wangechi (Kenya), Ali Kiba (Tanzania), Victoria Kimani (Kenya), Maurice Kirya (Uganda), Dama Do Bling (Mozambique) pamoja na Ice Prince (Nigeria).
Mbali na Ali Kiba kufanya kolabo ya Coke Studio na Ne-Yo, pia alifanya naye kolabo nje ya shoo hiyo. Kiba akiwa bado yupo nchini Kenya kwa shoo hiyo huku nyuma Diamond, Prodyuza Sheddy Clever pamoja na Sallam walitimba nchini humo na kufanya kolabo na Ne-Yo kimyakimya na meneja huyo akatupia picha mitandaoni jambo linalotafsiriwa kuchochewa na Sallam kujibu mapigo.

Septemba, 2016
Sherehe ya kutimiza miaka 10 ya Chama cha Orange for Democratic Movements (ODM) cha Raila Odinga, iliwaalika wakali Ali Kiba na Diamond bila kujuana katika Viwanja vya Mama Ngina, Mombasa.

Diamond alitangazwa kama msanii rasmi atakayetumbuiza bila kujua kama Kiba naye alikuwa ameingia nao ubia wa kulipwa kufanya shoo hiyo.
Diamond alipomaliza kupafomu, Kiba naye aliingia kama msanii sapraizi jambo lililofanya shangwe kuzidiana na kuonekana kama mmoja amefunikwa.

Kupitia ukurasa wa Instagram, Sallam aliandika maneno yaliyotafsiriwa hakufurahishwa na shoo ya kushtukiza iliyofanywa na Kiba ambapo alisema;
“Diamond ndiye msanii mkubwa aliyealikwa, nyomi ile haikuvutwa na msanii sapraizi (Ali Kiba). Asanteni Mombasa”

Pia akaweka picha na kuandika posti nyingine kuwa;
“Tumemaliza kufanya shoo Mombasa kinachofuatia ni ziara ya Afrika, hivyo kama kuna yeyote unamfahamu ni msanii sapraizi mtaje hapa.”

Oktoba 22, 2016?
Katika Tuzo za MTV (MAMA) zinazotarajiwa kufanyika Oktoba 22, mwaka huu, Ali Kiba amepangwa kutumbuiza. Tayari katika mahojiano aliofanyiwa, Sallam hivi karibuni ameweka wazi lazima atakuwepo backstage na Kiba asiogope kwani yeye ni mtu wa kawaida sana.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger