Oct 19, 2016

Bodi ya Wadhamini CUF yafungua kesi dhidi ya Jaji Mutungi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

BODI ya Baraza la Wadhamini la Chama cha Wananchi (CUF), imefungua kesi dhidi ya Jaji Francis Mutungi, George Masaju, Profesa Ibrahimu Lipumba na wafuasi 12 waliotimuliwa na chama hicho katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Jaji Mutungi ni Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Masaju ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Prof. Lipumba ni Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.

Bodi hiyo imefungua kesi hiyo ikiwa ni wiki chache baada ya mahakama hiyo kutoa kibali cha kufungua kesi dhidi yao.

Kibali hicho kilitolewa mbele ya Jaji Ama Isario Munisi ambapo alisema, mahakama ilijiridhisha kwamba, maombi ya bodi hiyo yaliyokuwa na hati ya kiapo cha Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad zipo sahihi, hivyo wanapaswa kufungua kesi hiyo ndani ya siku 14.

Hatua ya bodi kukimbilia mahakamani inatokana na kuibuka kwa mgogoro ndani ya chama hicho baada ya Prof. Lipumba kutangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti Agosti 6, mwaka jana na Juni mwaka huu, kutangaza kutengua barua yake na kisha kurejea kwenye wadhifa wake.

Bodi hiyo inayowakilishwa na mawakili zaidi ya 10 akiwemo Juma Nassoro, Hashimu Mziray na Twaha Taslima leo wamefanikiwa kufungua kesi iliyopokelewa na kupatiwa namba 23 ya mwaka 2016 chini ya hati ya dharura.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua kesi hiyo, Wakili Mziray amesema msingi wa kesi yao umejengwa katika hoja kubwa tatu ambazo;

Bodi imeiomba Mahakama Kuu kutengua barua ya Jaji Mutungi ya Septemba 23, mwaka huu iliyotengua uamuzi halali wa CUF, kumfuta uanachama Prof. Lipumba.

Pia bodi inaiomba mahakama hiyo kumzuia Jaji Mutungi kuendelea kufuatilia suala la CUF baada ya kupitishwa kwa uamuzi wa kumfuta uanachama Prof. Lipumba kwa kuwa, suala lake limefanyika kihalali.

Aidha katika hoja ya tatu, wanaiomba mahakama kumzuia rasmi Jaji Mutungi kutoingilia masuala yanayoihusu CUF, badala yake afanye kazi zinazomuhusu kisheria.

Badaa ya kueleza hayo, Wakili Mziray amesema sababu ya kufungua kesi hiyo chini ya hati ya dharura inatokana na hatari iliyopo ndani ya chama hicho.

“Licha ya kuwa kuna mambo yaliyotokea ndani ya chama, lakini kuna sababu ya kufungua kesi chini ya hati ya dharura kutokana na Ofisi Kuu ya chama pale Buguruni imekaliwa na watu ambao sio wanachama,”anasema na kuongeza;

“Lengo la chama ni kudhibiti ofisi zake zote katika hali ya usalama ikiwemo Makao Makuu, kwani Kaimu Katibu Mkuu anahitaji kusimamia kazi na shughuli za chama akiwa huru.”

Mbarara Maharagande, aliyeteuliwa kushika nafasi ya Unaibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano wa CUF amesema kuwa, chama hicho kinasikitishwa na utendaji kazi wa Jeshi la Polisi kwa kuwalinda na kuwaachia wahalifu wanaoivuruga CUF, badala yake inawakamata wasiohusika.

“Tunashangaa kuona polisi wanaharakisha kuwafikisha mahakamani wafuasi 23 waliokuja kuongeza nguvu ya kukilinda chama wakitokea Zanzibar, huku wakishindwa kuwachukuliwa hatua waliofanya tukio la utekaji ambalo ndio la kwanza kutokea,” anasema.

Maharagande anasema kutokana na hatua hiyo, asubuhi ya leo viongozi wa chama hicho wamekwenda Ofisi za Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Biswaro Mganga kuulizia hatma ya wafuasi waliohusika na tukio la utekaji iwapo wamechukuliwa hatua.

“Licha ya kufika ofisi hapo tumeshangazwa kuona hata kwenye orodha ya jalada la kesi za leo hakuna majina ya washtakiwa hao, licha ya kuwa wamekamatwa muda mrefu lakini wameshindwa kuchukuliwa hatua,” amesema



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger