Oct 19, 2016

BAVICHA: Nini hatma ya Vijana waliokosa mikopo ya Elimu ya Juu?

Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa kuwa utawala huu wa Serikali ya CCM, chini ya Rais John Magufuli zaidi ya nusu ya wanafunzi waliodahiliwa kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu mwaka wa masomo 2016/2017, wako katika hatari ya kukosa fursa ya kupata elimu hiyo kwa sababu ambazo hazieleweki hadi sasa.

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari na vyanzo vingine, Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) imeweza kudahili takriban wanafunzi wapya 58,000 kwa ajili ya elimu ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini kwa mwaka huu wa masomo.

Lakini katika hali ambayo tunajua itaumiza vijana wengi na kuwasikitisha Watanzania, taarifa ambazo zimethibitishwa na Serikali ya Rais Magufuli kupitia kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo, ni kwamba zaidi ya nusu ya idadi hiyo ya waliodahiliwa na TCU kusoma elimu ya juu, hawatapata mikopo!

Hivyo ndoto za kutafuta mafanikio yao, kwa ajili ya jamii zao na taifa letu kwa ujumla zinaelekea kukatiliwa. Hili ni jambo kubwa na zito kwa sababu linagusa moja ya misingi muhimu ya taifa lolote lenye ndoto ya kutaka kuendelea, achilia mbali kuwa taifa lenye uchumi wa kati unaotegemea viwanda.

Kwa mujibu wa Gazeti la The Guardian la Oktoba 18, mwaka huu, Serikali ya CCM, chini ya Rais Magufuli imesema itawakopesha wanafunzi wapatao 24,000, idadi ambayo haifiki hata nusu ya wanafunzi wote waliodahiliwa na TCU.

Hata hivyo kauli hiyo ya Mkurugenzi wa Bodi, tumeichukulia kuwa si ya kweli hata kidogo, bali ya mtu anayejaribu kuficha mambo kwa ajili ya “nusu shari kuliko shari kamili”.

Tunasema hivyo kwa sababu hadi sasa Bodi hiyo hiyo, imeshatoa mikopo kwa wanafunzi 3,966 tu. Idadi hiyo ni sawa na asilimia 6 tu kati ya wanafunzi wote waliopata udahili wa kusoma elimu ya juu kwa mwaka huu.

Maana yake ni kwamba kuwakopesha vijana wapatao 24,000 ili wasome elimu ya juu bado nayo ni ahadi tu ya maneno, lakini uhalisia uliopo kwa vitendo hadi sasa ni kwamba Serikali ina uwezo wa kuwakopesha vijana wake 3,966 pekee nchi nzima.

Idadi hiyo ambayo serikali imeweza kuwakopesha mikopo, haifiki hata nusu ya jumla ya wanafunzi wanaopaswa kudahiliwa na mojawapo ya vyuo vikuu vikubwa nchini, mathalani Chuo Kikuu Dar es Salaam.

WAMEKOPESHWA CHAKULA NA KULALA, SI KUSOMA!
Aidha, kwa muda mrefu sasa, walau tangu kuanza kwa utaratibu wa serikali kuwakopesha wanafunzi kwa ajili ya elimu ya juu, inaeleweka kuwa HESLB imekuwa ikitoa mikopo kwa ajili ya vitu vitatu; ada, malazi na chakula.

Katika hali ambayo inazidi kushangaza na kuibua maswali kuwa kuna jambo kubwa ambalo linafichwa, BAVICHA tunazo taarifa kuwa hata hao wanafunzi asilimia 6 ambao bodi inadai imeshawapatia mkopo, katika vyuo vingi wamepata fedha kwa ajili ya CHAKULA NA KULALA tu.

Hawajalipiwa fedha ya ada (tuition fees hadi sasa).
Kwa mantiki hiyo ni kwamba, Serikali ya CCM, chini ya Rais Magufuli hadi sasa wiki ya tatu tangu vyuo vifunguliwe si tu kwamba imeshindwa kuwakopesha wanafunzi wote wanaostahili kupata mkopo kwa ajili ya elimu ya juu, bali hata imeshindwa hata kulipa fedha za ada kwa wanafunzi ambao tayari imeshawakopesha. Hali hii ikiendelea tutegemee kuona vyuo vikuu na taasisi zingine za elimu ya juu vikifungwa kwa sababu vitakuwa haviwezi kujiendesha.

Taarifa hizi za Bodi ya Mikopo zinapaswa kulishtua taifa letu na kila Mtanzania aone jinsi ambavyo Serikali ya CCM chini ya Rais John Magufuli haijajipanga na wala haijui inachokifanya katika kuhakikisha inatoa elimu bora kwa Vijana wetu.

Lakini pia zinathibitisha kuwa Serikali ya Rais Magufuli iko katika hali mbaya ya kifedha na hivyo inahitaji msaada wa fikra mpya nje ya CCM kuikwamua vinginevyo tujiandae kwa mwendelezo wa janga kubwa zaidi katika sekta ya elimu.

Tunamtaka Rais John Magufuli kujitokeza hadharani, na kuueleza umma wa Watanzania hatma ya Vijana waliokosa mikopo, na kama ahadi zake alizozitoa wakati wa Kampeni zilikuwa ni ulaghai au ghiliba za kutafuta kura?

Pia Rais Magufuli anapaswa kuwaeleza watanzania ikiwa ameshindwa utekelezaji wa ahadi zake ikiwemo Elimu bora, au akubali kuwa yeye ni Muongo kwa sababu wakati wa kampeni alisema nanukuu; “ETI NIWE RAIS HALAFU NISIKIE WANACHUO WAMEKOSA AU WAMECHELWESHEWA MIKOPO YAO, WATANIJUA MIMI NI NANI, KITU CHENYEWE KINAITWA MIKOPO HALAFU UNACHELEWESHA” Mwisho wa kunukuu.

Tunawataka Viongozi wa serikali za wanafunzi katika Vyuo Vikuu vyote nchini, kuungana pamoja ili kudai haki ya wanafunzi wenzao, tukitambua kuwa, baadhi ya Viongozi wa shirikisho la serikali za wanafunzi wa elimu ya Juu (TAHILISO) wamekuwa wakitumika kwa ajili ya CCM badala ya maslahi mahsusi ya wanafunzi na hivyo kuidhoofisha taasisi hii muhimu ya wasomi, hivyo umoja wao ni muhimu katika kuipata haki hii.

Tunatoa wito kwa taasisi mbalimbali za kutetea haki za vijana, asasi za vijana pamoja na mtandao wa wanafunzi Tanzania, kujitokeza hadharani na kuwapigania vijana hawa katika kuhakikisha wanapata haki yao ya msingi ya elimu.

Imetolewa leo Jumatano,19.10.2016
Patrobas Katambi
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger