Oct 8, 2016

Ndanda yatishia kujiondoa Ligi Kuu


Mtwara/Dar. Timu ya soka ya Ndanda FC ya mkoani Mtwara, imetishia kujitoa katika Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara inayoendelea kutokana na kukabiliwa na ukata.

Akizungumza na gazeti hili jana, Ofisa Habari wa timu hiyo, Idrisa Bandali alisema kuwa hali ya uchumi katika klabu hiyo ni ngumu hivyo watu wasishangae kuiona timu ikishindwa kuendelea na ligi.

“Tuko katika wakati mgumu, hatuna fedha za kulipa wachezaji mishahara na hata shughuli za klabu na timu za kila siku.

“Mfano mdogo tu, hivi karibuni tulilazimika kulala Dumila, Morogoro tukitokea Mwanza baada ya kuchelewa kuondoka kutokana na kukosa fedha ya kulipia hoteli.

“Kuna wakati nimekuwa nikiomba wanahabari watusaidie kuifanya Ndanda kuwa ajenda katika vyombo vyao ili tupate msaada lakini hali bado ni mbaya.

“Ninataka kuwaambia msishangae kuona Ndanda ikishindwa kuendelea na ligi licha ya kuwa bado tuna mechi za ugenini na tunafahamu tutakapokosa, adhabu mojawapo ni kushushwa daraja,” alisema Bandali.

Kanuni za Ligi Kuu
Kwa mujibu wa Kanuni ya 27 ya Ligi Kuu kifungu cha nne, klabu yoyote itakayojitoa kwenye Ligi Kuu baada ya Ligi kuanza au kushindwa kucheza mchezo mmoja wa ratiba ya Ligi Kuu katika msimu itakabiliwa na adhabu zifuatazo:

(a) Itashushwa daraja na kufungiwa kucheza Ligi kwa misimu miwili, Bodi ya Ligi Kuu pia inaweza kuichukulia hatua zaidi klabu hiyo/viongozi au wachezaji iwapo itathibitika kuwa imejitoa kwa madhumuni ya kuhujumu msimamo wa Ligi au hujuma nyingine yoyote.

(b) Iwapo itajitoa au kushindwa kumaliza Ligi kwa sababu yoyote ile, timu zaidi ya idadi ya timu za kushuka daraja kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu, zote zitashuka daraja (kanuni 25:4a) na timu zaidi zitapanda kutoka daraja la kwanza (FDL) ili kujaza nafasi na idadi ya timu za Ligi Kuu kuendelea kuwa ilivyokusudiwa.

Kipengele (c) kinasema matokeo ya michezo yote iliyowahi kuchezwa itafutwa lakini kitakuwepo kwenye orodha ya msimamo wa ligi.

Kwa mujibu wa kanuni hizo kipengele (e), timu itapoteza haki zake zote stahili kwa timu za Ligi Kuu na itawajibika kurejesha stahili yoyote iliyokwishachukua kabla ya kujitoa endapo itaamriwa kufanya hivyo kutokana na mazingira ya kujitoa kwake.

Licha ya kutoa tishio hilo huku ikicheza na African Lyon leo, Ndanda FC ilikwishacheza na Simba na kufungwa mabao 3-1, ilifungwa na Mbao FC mabao 2- 0 kabla ya kufungwa mabao 2-1 na Mtibwa Sugar.

Mechi ambazo Ndanda yenye pointi 11, ilishinda ni dhidi ya Majimaji na Azam 2-1 na ile ya Toto Africans bao 1-0. Ndanda ilitoka suluhu mechi za Yanga na Kagera Sugar.

“Kwa sasa hatuna mdhamini yoyote zaidi ya Azam anayedhamini ligi na kwamba tunaendeshwa kwa michango ya viongozi na wahisani mbalimbali ambao hujitolea kwa kiasi ambacho bado hakijitoshelezi.

“’Kuendesha timu ni kazi ngumu, hali yetu ni mbaya ndio maana wakati mwigine tunashindwa kulipa mishahara kwani pia kuna wachezaji ambao bado hawajamaliziwa pesa za usajili zinazofikia Sh30mil kwa msimu huu wa 2016/2017,” alisema Bandali

Ligi Kuu yaendelea
Wakati hali ikiwa hivyo kwa Ndanda FC, ligi hiyo inaendelea leo kwa Mtibwa Sugar kuwa ugenini dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi wakati Majimaji itaikaribisha Mbao kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Majimaji inayonolewa na Kally Ongalla, inashika mkia kwenye ligi na itakuwa na kazi ngumu leo kupambana na Mbao ambayo imeizinduka katika siku za karibuni.

Ongalla alisema ana wakati mgumu kurejesha morali ya wachezaji wake ili warudi katika kiwango bora lakini anaamini mchezo wa leo watapata matokeo mazuri.

Kocha wa Ndanda, Said Mohamed alitamba kuiadhibu Lyon kama alivyoifanyia Toto African wiki iliyopita.

Naye kocha wa maafande wa JKT Ruvu, Malale Hamsini alisema anaijua shughuli ya Mtibwa Sugar hivi sasa na amekiri kuwa kazi itakuwepo leo huku Kocha wa Mtibwa Sugar, Salum Mayanga akisema wamejindaa vizuri kuhakikisha wanashinda mchezo huo.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger