Tahadhari hiyo imetolewa na Afisa Utumishi wa CWT-taifa,Bw Ali Shabani kwa niaba ya Katibu wa CWT-taifa Bw Yahaya Msulwa wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa Ofisi ya Chama hicho ya wilaya pamoja na kuwakabidhi mabati 360 walimu 36 waliostaafu mwaka huu ili kukabiliana na maisha yasiyotegemea ujira,huku akidai kwamba kutokana na kufikishwa kwa malalamiko hayo ya utapeli kwenye vyombo vya dola lazima wastaafu kuwa makini.
Awali akitoa taarifa ya wilaya ya Kondoa,Katibu wa CWT Bw Darabe amesema licha ya walimu kudai deni la zaidi ya shilingi Mil.335 lakini pia walimu 718 waliopandishwa madaraja kwa mwaka 2016/17 wanalalamikia kunyang’anywa kwa madaraja yao,huku Afisa Utumishi wa halmashauri ya mji wa Kondoa bw Pepino Mfugale akikanusha madai hayo.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment