Nov 6, 2016

Bodi ya Mikopo yacharuka..Wanaodaiwa Kukamatwa na Kulazimishwa Kulipa Deni

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imewapa siku 30 kuanzia Novemba 14, mwaka huu wadaiwa wake sugu 154,000 kurejesha fedha wanazodaiwa.

Vinginevyo, imesema watakamatwa na kulazimishwa kulipa madeni na gharama za kuwasaka.

Kwa mujibu wa bodi hiyo, wadaiwa wote wanaoangukia katika mkumbo huo, watatangazwa katika vyombo mbalimbali vya habari Novemba 13, siku moja kabla ya kuanza kwa notisi hiyo ya siku 30, isipokuwa kwa wale ambao watakuwa tayari wamelipa.

Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul Razaq Badru alisema wadaiwa hao ni wa kuanzia mwaka 1994 mpaka sasa ambao madeni yao yameiva.

Alisema hadi sasa serikali inadai Sh trilioni 2.6 kutoka kwa wadaiwa hao ambao walikopeshwa kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu lakini hawajarejesha mikopo hiyo na hivyo kuleta changamoto kwa waombaji wapya.

“Bodi itatangaza majina ya wadaiwa sugu wa kuanzia mwaka huo ambao madeni yao yameiva, majina yao tutayaweka hadharani Novemba 13, mwaka huu baada ya hapo tutawapa siku 30 kulipa, baada ya muda huo, hatua za kisheria zitachukuliwa na wahusika watalipia gharama za kuwasaka,” alisema Badru.

Alisema wadaiwa hao sugu wanapaswa kukumbuka kuwa kutolipa madeni yao ni kuvunja Mkataba na Sheria ya Bodi hiyo Namba 9 ya mwaka 2004, 19 (1).

Sheria hiyo ya mwaka 2004 Kipengele cha pili kinasema mdaiwa atapewa penalti ya asilimia tano juu ya ile asilimia tano iliyokuwa ikitozwa kabla, kwa kila mwezi kwenye deni lililobakia au alilonalo. Aidha, kipengele cha tatu kinasema mdaiwa ataongezewa gharama za kumtafuta alipo ili alipe deni lililoingiwa na bodi.

Vipengele vingine kwenye sheria hiyo vinasema mdaiwa atawekwa kwenye orodha ya wadaiwa sugu ‘blacklist’ na maelezo yake yatapelekwa kitengo cha kumbukumbu ya wakopaji na hivyo kushindwa kukopa sehemu nyingine yoyote.

Pia mdaiwa atazuiliwa kupata udhamini wa serikali au udahili wa masomo ya juu kwenye vyuo vyovyote ndani na nje ya nchi. Kadhalika, maelezo yao yatapelekwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Kitengo cha Uhamiaji na balozi zote ambako watakataliwa safari zozote za kwenda nje ya nchi.

Badru alisema awali selikali ilitoa mikopo hiyo kwa wanafunzi, kwa kuweka bayana kwamba fedha walizopewa ni mikopo na wala si msaada au ruzuku, hivyo zinapaswa kujereshwa mara baada ya mdaiwa kuhitimu masomo yake; au pindi atakapositisha masomo yake kwa sababu mbalimbali.

Kuanzia mwaka wa masomo wa 1994/95 mpaka 2004/05, mikopo ilitolewa kwa wanafunzi kwa ajili ya kugharimia chakula na malazi pekee. Lakini kuanzia mwaka 2005/06 mpaka sasa, pamoja na gharama ya chakula na malazi, wanafunzi wanakopeshwa pia fedha kwa ajili ya kugharimia ada ya mafunzo, vitabu , viandikwa, mafunzo kwa vitendo, mahitaji maalumu ya vitivo na gharama za utafiti.

Akizungumzia ulipwaji wa fedha za mikopo kwa wanafunzi wanaoendelea na masomo, Badru alisema jana (juzi) walisambaza katika vyuo vyote nchini zaidi ya Sh bilioni 71 kwa wanafunzi hao.

Usambazaji huo umefanyika baada ya vyuo vya elimu ya juu 13, kuwasilisha matokeo ya wanafunzi wake, kama walivyoamriwa na wizara husika na kwamba vyuo viwili pekee, ndivyo bado havijawasilisha matokeo.

Pamoja na vyuo hivyo kutowasilisha matokeo hayo, bodi imewapelekea wanafunzi hao fedha na kwamba bodi itashughulika na vyuo husika kiutawala ili kuepusha wanafunzi hao kushindwa kuendelea na masomo.

“Wote tumewawekea fedha katika akaunti za vyuo jana usiku (juzi) kwa utaratibu maalumu kuhakikisha wanafunzi wanaoendelea na masomo katika vyuo mbalimbali wanapata fedha zao,” alibainisha Badru.

Hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Maimuna Tarishi alivipa siku 15 vyuo vilivyokuwa havijawasilisha matokeo ya wanafunzi wanaoendelea na masomo, kuwasilisha ifikapo Novemba 2, mwaka huu.

Vyuo hivyo vilivyokuwa viwasilishe matokeo hayo siku 30 kabla ya kufunguliwa na kwamba utaratibu ni lazima vyuo kuwasilisha matokeo kuonesha wanafunzi wangapi wana sifa za kuendelea kupewa mikopo.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger