Akizungumza katika mkutano huo mwenyekiti wa machinga Said Tembo amesema wao kama machinga wako tayari kwa lolote hata kama ataanza leo oparesheni yake atawakuta wapo katika maeneo yao ya biashara na hakuna mtu yeyote atakayeondoka katika eneo la biashara.
Mwenyekiti huyo amesema wao kama wafanyabiashara wanasimamia kauli ya Rais aliyoitoa juu ya machinga kutokuondolewa mjini badala yake watengewe maeneo mengine ambayo yako katikati ya mji na si nje ya mji kama alivyofanya mkuu huyo na kuongeza kuwa Raisi akitoa kauli siku zote kauli hiyo huwa sheria.
Moja kati ya machinga akizungumza katika mkutano wao
hata hivyo machinga hao wamesema hawako tayari kuondoka kwa sababu hakuna makubaliano yoyote yaliyofanyika kati yao na serikali ili kufikia muafaka wa jambo hilo hivyo wanaisubiri siku hiyo ifike ili wajue mwanzo na mwisho wao.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment