Nov 21, 2016

Mambo 10 Yanayotia Doa Utawala wa JPM


Dar es Salaam. Serikali ya Awamu ya Tano imefanya vizuri katika mwaka wake wa kwanza, ikifanikiwa kurejesha nidhamu ya kazi kwa kiasi kikubwa, kupambana na ufisadi, kukusanya mapato ya Serikali na kuwawajibisha bila aibu viongozi na watumishi wa umma.

Ununuzi wa ndege mbili, malipo yaliyofanikisha awamu ya pili ya mradi wa umeme wa Segerea, kuanzisha mahakama ya mafisadi, kuzuia matumizi yasiyo ya lazima kwa kufuta sherehe za maadhimisho ni kati ya mambo yaliyofurahiwa na wengi.

Lakini, wakati Rais John Magufuli na Serikali yake wakianza mwaka wa pili, baadhi ya wasomi na wanasiasa wamemshauri Rais Magufuli afanyie kazi mambo 10, likiwamo la mchakato wa Katiba mpya ambalo alisema si kipaumbele chake.

Mbali ya Katiba, wachambuzi hao walitaja mambo mengine muhimu yanayopaswa kufanyiwa kazi kuwa ni kuangalia uwezekano wa kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera, hali ya siasa Zanzibar, kuheshimu sheria wakati wa kuwajibisha watumishi, kuruhusu uhuru wa mihimili ya nchi, kuruhusu demokrasia, kuruhusu shughuli zote za Bunge kuonyeshwa moja moja na vituo vya televisheni na redio na kuepuka kauli tata.

“(Rais Magufuli) Amefanikiwa katika mapambano dhidi ya rushwa, kuwafanya watu wapende na kuheshimu kazi. Sasa atakavyomaliza na kuondoka, haya yote yataachwa ikiwa hatasimamia mchakato wa Katiba mpya,” alisema mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu, Dk Hellen Kijo-Bisimba.


Katiba Mpya

Ilani ya CCM inazungumzia mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa shughuli za Serikali kwa kipindi cha 2010-2015 kuwa ni pamoja na mchakato wa kuandika Katiba mpya kuendeshwa na kufikia hatua ya kupigia kura Katiba Inayopendekezwa baada ya kupitishwa na Bunge maalumu.

Akipokea ripoti ya Uchaguzi Mkuu Juni 23, Magufuli alisema mambo fulani yataongezeka katika Katiba Inayopendekezwa, lakini Novemba 4 alipozungumza na wahariri wa vyombo vya habari alisema hakuwahi kuzungumzia Katiba wakati wa kampeni zake kwa hiyo si kipaumbele chake, na kwamba anachotaka kwanza ni “kunyoosha nchi”, kauli inayotafsiriwa kuwa ni kuisigina Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Kushughulikia maafa ya Kagera

Suala jingine ambalo wachambuzi wamelizungumzia ni jinsi Serikali ilivyoshughulikia tetemeko la ardhi lililoikumba mikoa ya Kanda ya Ziwa na hasa, Kagera ambako takribani watu 17 walipoteza maisha, zaidi ya nyumba 840 kubomoka na nyingine 1,264 kuharibika.

Kutokana na janga hilo, Septemba 11, Rais Magufuli aliahirisha ziara ya siku tatu nchini Zambia ambako pamoja na mambo mengine, angehudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Edgar Lungu.

Septemba 18 wakati akipokea taarifa ya maafa yaliyosababishwa na tetemeko hilo kutoka kwa Waziri Mkuu, iliyoeleza kuwa zilikusanywa Sh3.6 bilioni, Rais Magufuli alisema Serikali itarekebisha miundombinu iliyoharibiwa na tetemeko na kuwataka waliobomolewa nyumba, wajipange kuzirekebisha. Serikali ilizuia watu au taasisi kutoa misaada kwa waathirika, badala yake ikaagiza wapitie Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ambaye hivi karibuni alikaririwa akisema kipaumbele itakuwa ni ujenzi wa miundombinu na taasisi za serikali.

Maamuzi ya haraka

Serikali inadaiwa kuwajibisha wakuu wa idara kabla tuhuma dhidi yao kuthibitishwa. Baadhi yao walisimamishwa au kufukuzwa kazi katika mikutano ya hadhara na wengine wakati wanaendesha vikao. Jambo hili limekuwa likifanywa hata na wakuu wa mikoa na wilaya kwa kuwaweka mahabusu watu walio chini yao.

Kuzuia mikutano ya siasa

Dosari nyingine ni kutofuata Katiba, Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Utumishi wa Umma. Rais amezuia mikutano ya siasa na maandamano. Kwa kuwa Sheria hizo zinaruhusu, Jeshi la Polisi linatekeleza zuio hilo kwa maelezo kwamba ina viashiria vya kuvunja amani au kuibuka kwa magonjwa.

Pia, Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Na 1 wa mwaka 1992 uliorudiwa mwaka 2015 umewazuia askari kujihusisha na siasa, lakini wengi wamepewa nyadhifa za siasa.

Sakata la Zanzibar

Pia, hali ya kisiasa Zanzibar ni jambo jingine lililozungumzwa na wachambuzi. Wakati akilihutubia Bunge Novemba 20 mwaka jana, Rais Magufuli alionyesha uwezekano wa kuutafutia ufumbuzi mkwamo wa kisiasa Zanzibar na baadaye kuwa na mazungumzo na katibu mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad Desemba 21. Lakini hotuba mbili alizotoa katika ziara ya Pemba Septemba 2 na Unguja Septemba 3, Rais Magufuli aliondoa uwezekano wa kupatanisha makundi hasimu ya kisiasa kati ya CCM na CUF, jambo ambalo limekosolewa na wengi.

“Zanzibar imeathirika sana, yale matumaini ya kuweka mfumo mpya kupitia Katiba Mpya ya Jaji Joseph Warioba yamepotea lakini hata mipango ya kuimarisha Serikali ya Umoja wa Kitaifa imepotea,” alisema mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar, Profesa Abdul Sherrif. “Uchaguzi  Zanzibar umeacha mpasuko wa wananchi badala ya kuwaunganisha.”

Matamko ya ghafla

Jambo jingine lililogusa wengi ni kufuta sherehe za maadhimisho na baadhi katika dakika za mwisho. Mfano ni uamuzi wa kuzuia wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi na maofisa wengine kwenda Simiyu kuhudhuria hafla ya kuzima Mwenge wa Uhuru, wakati baadhi  walishafika na wengine wakiwa safarini.

Rais Magufuli aliwaambia maofisa wote waliofika Simiyu au waliokuwa njiani kurudi katika vituo vyao vya kazi na kurejesha fedha walizotumia.

Pia, Rais amekuwa akitoa kauli zinazodaiwa tata ambazo baadhi zinaweza kuwa na madhara kama kuwataka askari wa usalama barabarani kuondoa tairi za gari wanalokamata, au kuwapa polisi fedha za kubrashia viatu.

Bunge ‘live’

Suala jingine ni Bunge kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya shughuli za Bunge tofauti na ilivyokuwa katika Bunge la Tisa na la Kumi.

Kudhibiti mihimili

Ingawa Serikali ndiyo ina wajibu wa kutafuta fedha, Mahakama na Bunge ni mihimili inayojitegemea. Mwishoni mwa mwaka jana, Rais anadaiwa kuagiza fedha za sherehe ya kuwapongeza wabunge zitumike kununulia vitanda kwa ajili ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), na mapema mwaka huu, aliiomba mahakama imalize kesi za kodi ili Serikali ipate Sh1.4 trilioni na kuupa mhimili huo sehemu ya fedha hizo.

Mambo mengine

Mambo mengine ambayo yametajwa kutia doa mwaka mmoja wa Serikali ni nidhamu ya uoga kwa watumishi wa umma pamoja na kuyumba kwa hali ya kifedha miongoni mwa Watanzania jambo ambalo linaonekana kulalalamikiwa na makundi karibu yote.

Maoni ya wachambuzi

Wachambuzi waliohojiwa na gazeti hili kuhusu masuala hayo, walikuwa na maoni tofauti.

Dk Kijo-Bisimba, ambaye ni mwanasheria, alisema Katiba mpya ndiyo msingi wa kuwaongoza watawala kwa sababu inabeba yale yote ya msingi yanayotakiwa kutekelezwa bila kuvunja haki za binadamu.

“Rais ahakikishe Katiba mpya inapatikana, ile yenye maoni ya wananchi. Pia, awaache wanasiasa kwa sababu kitendo cha kuzuia mikutano kinawafanya wapate ya kuzungumza. Kama akiwaacha na yeye akasimamia Katiba na kutekeleza majukumu yake hawatapata jambo la kuzungumza,” alisema.

Mbunge wa Makete (CCM), Profesa Norman Sigalla alisema Rais Magufuli amefanya vizuri na kukifanya chama chake kiendelee kuaminika.

Hata hivyo, alisema ni vizuri aifanye Serikali yake iwapende matajiri wanaopata fedha zao kwa halali badala ya kuwaona fisadi.

“Baadhi ya wawekezaji wakisikia kwamba kila mwenye fedha Tanzania anaitwa fisadi, hawawezi kuja kuwekeza; vivyo hivyo matajiri hawawezi kuweka fedha kwenye mabenki yetu kwa sababu wanahofia kuonekana mafisadi,” alisema.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili, Dk Ave Maria Semakafu alisifu utumbuaji wa majipu akisema umesaidia kuwashtua baadhi ya watendaji waliokuwa wakifanya kazi kwa mazoea.

Lakini alisema suala la Katiba mpya linapaswa kusubiriwa kwa muda badala ya kukurupuka.

Dk Semakafu alisema kilichokuwa kikipigiwa kelele zaidi kwenye Katiba ni viongozi kutowajibika na kukosa uadilifu, huku wachache wakinufaika na keki ya Taifa.

“Tuendelee kuona mwelekeo wa Rais Magufuli kwanza ndipo suala la Katiba lianze. Ikumbukwe kuwa kilichokosekana wakati ule ni suala usimamizi madhubuti ambao hivi sasa umeonekana,” alisema.

Kilio cha Dk Semakafu katika kipindi cha mwaka mmoja wa utawala wa Rais Magufuli ni suala la usawa wa kijinsia ambalo anasema nafasi za wanawake zimepungua, hasa katika ngazi za kufanya maamuzi.

“Idadi ya wanawake kwenye ngazi ya maamuzi imerudi nyuma, hili nalo litapaswa kupewa msukumo wa kikatiba muda utakapofika ili wanawake na wanaume wote kwa pamoja wahusike kwenye ngazi hii muhimu,” alisema.

Lakini mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Peter Msigwa alisema Rais Magufuli ameonyesha kutovumilia kukoselewa.

Mchungaji Msigwa pia alisema kuzuia mikutano ya Bunge kuonyeshwa ‘live’, kuzuia mikutano ya hadhara ya siasa na kubana vyombo vya habari kunaashirisha kwamba hapendi kukoselewa.

“Maana yake ni kwamba wananchi wakifuatilia Bunge wataona hoja nzito zinavyojibiwa. Pia wanasiasa ndiyo wanaoweza kuzibua masikio ya Watanzania. Rais wetu hapendi kupata maoni na kukosolewa,” anasema.

Pia, alisema katika kipindi hicho Rais Magufuli ameonekana kushindwa kujibu kwa ufasaha maswali ya waandishi wa habari, jambo ambalo alisema ni udhaifu.

Hata hivyo, akizungumza na wahariri, Rais Magufuli alisema anapenda kukosolewa na anafanyia kazi ukosoaji hasa ule unaozingatia weledi.

Mwananchi



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger