Nov 14, 2016

Rais Magufuli Aitosa Mialiko ya Sh5 Bilioni

Kitendo cha Rais John Magufuli kukataa mialiko 44 kati ya 47 ya nje ya nchi kimeokoa zaidi ya Sh5 bilioni na baadhi ya wasomi waliohojiwa kuhusu hatua hii wametofautiana. Wapo waliopongeza na wengine wakisema kusafiri kuna umuhimu mkubwa kwa Taifa.

Novemba 4, katika mahojiano na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, Rais Magufuli aliwaambia kuwa mwaka huu alipata mialiko 47 ya kusafiri nje ya nchi lakini aliamua kwenda mitatu.

Kwa mujibu wa makadirio yaliyofanywa na gazeti hili, Rais Magufuli ambaye amekuwa akisisitiza kuhusu kubana matumizi amefanikiwa kuokoa Sh5.7 bilioni.

Kiasi hicho cha fedha ni makadirio ya wastani wa fedha ambazo Rais Magufuli na msafara wa watu 50 ambao angeongozana nao wangetumia kwenye safari hizo 44 kwa siku tatu kila safari.

Katika fedha hizo, kwa makadirio ya wastani ya posho anayotakiwa kulipwa mtumishi wa Serikali anaposafiri nje nchi ni dola za Marekani 400 sawa na Sh872,000 kwa siku.

Hivyo endapo Rais Magufuli angesafiri nje ya nchi na wajumbe 50 kwa siku moja, wajumbe hao wangelipwa jumla ya Sh43,600,000.


Iwapo safari hiyo ingekuwa ya siku tatu, wajumbe hao 50 wangelipwa posho jumla ya Sh130,800,000.

Kiasi hicho cha fedha kikizidishwa kwa mialiko ya safari 44 ambazo Rais Magufuli hakwenda huenda akawa ameokoa Sh5.7 bilioni.

Taarifa ambazo gazeti limezipata kutoka katika vyanzo vya kuaminika zinaeleza kuwa kuna madaraja mawili ya malipo ya posho kwa watumishi wa Serikali wanaposafiri nje ya nchi.

Madaraja hayo ni A na B. Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, malipo ya posho kwa safari katika nchi za Bara la Ulaya na Amerika ambayo ni daraja A ni dola za Marekani 420 sawa na Sh915,600.

Malipo ya posho kwa safari za nchi za Bara la Asia na Afrika ambayo ni daraja B ni dola za Marekani 380 sawa na Sh828,400.

Vyanzo hivyo vimeongeza kuwa kuna mahitaji matano ambayo mtumishi anatimiziwa anaposafiri kwenda nchi ya nje ambayo ni fedha za suti, fedha za kujikimu na usafiri wa ndani atakapokuwa katika nchi husika. Pia, mtumishi anapewa ‘poketi money’ sanjari na kuongezewa posho endapo safari yake itazidi saa nane akiwa angani.



Mtazamo wa wadau

Akizungumzia hatua hiyo ya Rais Magufuli, Profesa wa uchumi, Chuo Kikuu cha Mzumbe, Honest Ngowi alisema kwa diplomasia ya uchumi hivi sasa, ni afya Rais kutoka kwenda nje hasa ikiwa safari hizo zitakuwa za mkakati kwa manufaa ya Taifa.

“Sijajua mialiko aliyotakiwa kwenda na akaikataa, lakini ni muhimu Rais akasafiri kwenda nje kujifunza na kubadilisha mawazo kama tunavyowapokea viongozi wengine hapa nchini,” alisema Profesa Ngowi.

Hata hivyo, Profesa Ngowi alisema hana taarifa za kiundani za aina ya mialiko aliyoikataa Rais Magufuli ili atoe maoni yake ya faida na hasara kwa kiongozi huyo wa nchi kukubali michache na kukataa mingi.

Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Benson Bana alisema safari za nje ya nchi si vipaumbele vya Rais Magufuli na kwamba ameamua kubaki nchini huku akiwakilishwa na viongozi walio chini yake ili kupunguza gharama.

“Huo ni uamuzi mzuri na ningemshangaa Dk Magufuli kama anawakataza viongozi walio chini yake wasisafiri nje ya nchi halafu yeye akawa anasafiri kila wakati,” alisema.

Alisema wa Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete alisafiri sana kwenda katika nchi mbalimbali ambako huko aliweka mtandao imara wa kidiplomasia.

“Sasa Magufuli akaona yeye aelekeze nguvu kufanya kazi za ndani ya nchi,” alisema.

Alisema hata nchi ambazo amezitembelea kama Rwanda ni kwa sababu kulikuwa na umuhimu wa kwenda yeye mwenyewe.

“Unakumbuka Rwanda walikuwa watumiaji wakubwa wa Bandari ya Dar es Salaam na walianza kujiondoa taratibu, katika mazingira kama hayo unatakiwa kwenda mwenyewe bila kuwakilishwa,” alisema.

Alisema hakuna umuhimu kwa Rais kwenda kwenye mikutano na badala yake aendelee kuwakilishwa na viongozi walio chini yake ili kupunguza gharama.

“Nampongeza kwa kuwa ameanza vizuri, ameenda Kenya na Uganda kwa kuwa wao ni majirani ambao ni wadau wakubwa katika diplomasia ya kiuchumi,” alisema.

Profesa wa Chuo Kikuu Katoliki Ruaha mkoani Iringa (Rucu), Gaudence Mpangala alisema kuna umuhimu kwa Rais kufanya ziara za nje ya nchi anakoalikwa na kuhudhuria mikutano mbalimbali ya kimataifa.

Alisema licha ya kuwa ziara za Rais huwa ni zenye gharama kubwa, lakini kuna umuhimu wa yeye mwenyewe kwenda huko badala ya kuwakilishwa na vingozi wengine.

Alisema: “Unapokutana na marais wenzako kuna umuhimu katika medani za kiuchumi kwa kuwa unakuwa na mamlaka ya kuzungumza kila jambo linalohusiana na nchi yako badala ya mtu anayekuwakilisha ambaye mambo mengine hawezi kuyajibu hadi apewe ruksa.”

Alisema tusifikirie gharama anazotumia na ujumbe wake kwenda nje ya nchi badala yake tufikirie pia faida zinazotokana na Rais mwenyewe kwenda nje ya nchi.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger