Nov 5, 2016

Wapinzani Wamsifu Rais Magufuli Wadai ana Ujasiri wa Pekeee


WABUNGE wa upinzani wamemwelezea Rais John Magufuli kuwa ni mtu mwenye ujasiri wa pekee ambao watu wengi hawana, kwani amefanikiwa kurejesha nidhamu na kupambana na rushwa.

Pia wamemwelezea Rais mstaafu Jakaya Kikwete kuwa ni kiongozi aliyeisaidia nchi kuendelea mbele katika eneo la uwekezaji na kutoa uhuru wa Watanzania kutoa maoni.

Wakichangia mjadala wa mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2017/2018 na mwongozo wa bajeti ya Serikali wa mwaka 2017/2018 juzi, bungeni mjini hapa, wabunge hao kwa nyakati tofauti walisema pamoja na kwamba si mambo yote anafanya vizuri, lakini Rais ni jasiri na ameweza kushughulikia rushwa.

Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema), alisema mtu atakuwa wa ajabu akikataa kutambua dhamira ya Rais ya kurejesha nidhamu na kupambana na rushwa. Alisema Rais amerejesha nidhamu, pia ameonesha dhamira njema katika kupambana na rushwa nchini lakini akataka anapokosea kwa kuwa naye ni binadamu, aambiwe.

“Rais anapofanya vizuri, aambiwe na anapokosea, aambiwe, kama nyie (akielekeza upande wanakokaa wabunge wa CCM na mawaziri) hamtamwambia, sisi tutasema,” alisema Msigwa.

Msigwa aligusa na kusifu utendaji kazi wa marais waliopita, kuanzia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere hadi Jakaya Kikwete, akisema walifanya mambo mazuri na Magufuli pia.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wa CCM walishangazwa kwa sifa hizo hasa kwa Rais Kikwete ambaye wapinzani walimbeza enzi akiwa madarakani na kudai nchi imemshinda. Mbunge wa Viti Maalum, Felista Bura (CCM) alisema wapinzani walikuwa wakisema Kikwete anachekacheka, hawezi kuongoza nchini.

“Walikuwa wanasema JK (Jakaya Kikwete) anachekacheka, leo wanamsifu?” alishangazwa Bura. Mbunge wa Jang’ombe, Ali Hassan King (CCM) alisema ikiwa sasa wapinzani wanaona Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete walikuwa wazuri, hata Magufuli watampenda tu na kumuona mzuri siku zijazo.

Nje ya ukumbi wa Bunge, wabunge wengine wa upinzani walizungumza na gazeti hili na kuunga mkono juhudi za wazi za kuimarisha nidhamu kwa watumishi wa umma na kupambana na ufisadi zinazofanywa na Rais Magufuli. Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF), alisema, “Ukweli lazima niseme yapo maeneo ambayo Rais amefanya vizuri na mengine bado”.

Sakaya alisema eneo la kuzuia mianya ya rushwa kwa kusimamia mapato, kubana fedha watu ambazo awali zilikuwa zikichezewa ovyo na kurejesha nidhamu ya kazi iliyopotea muda mrefu nchini, inapaswa ipongezwe.

Kwa upande wake, Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma (CUF), alisema utendaji kazi wa rais ni mzuri hasa eneo la kurejesha maadili na nidhamu katika kazi hasa kwa watumishi wa umma.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger