Dec 7, 2016

Kiama chaja: Uhakiki wa Vigogo Wenye Mali Nyingi za kufuru

Balaa jipya kwa vigogo wenye mali kufuru

SIKU moja baada ya Serikali kutangaza kuwa inaandaa uhakiki kabambe wa mali za viongozi wa umma takribani 500 nchini, imebainika kuwa operesheni ya sasa itakwenda mbali zaidi kwa kufichua pia mali zilizofichwa na wahusika kwa kuziandikisha majina yasiyokuwa yao.

Aidha, imefahamika vilevile kuwa operesheni hiyo itawaweka matatani watu wanaoonekana kuwa na utajiri kufuru ndani ya kipindi kifupi, lengo likiwa ni kufahamu kama hawatumiwi na baadhi ya vigogo kumiliki mali zilizopatikana kwa njia haramu kwa nia ya kukwepa mkono wa sheria.

Taarifa ya kuwapo kwa mkazo zaidi wa operesheni hiyo ya aina yake imeifikia Nipashe ikiwa ni siku moja baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki, kuutangazia umma juu ya kuwapo kwa uhakiki wa mali za viongozi wa umma kwa nia ya kujua kile walichojaza katika fomu zao na uhalisia wake.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na madai kuwa Sekretatieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma haina nguvu ya kutosha kuwabana
viongozi wanaojilimbikizia mali kwa kutumia vibaya madaraka yao huku wakiziandikisha mali zao kwa majina yasiyokuwa yao.

Hata hivyo, kupitia operesheni ya sasa, chini ya utawala wa awamu ya tano uliotangaza vita isiyokoma dhidi ya vitendo vya ufisadi, yaelekea hakuna tena mwanya wa kuficha mali kwa njia hiyo ya kuziandikisha kwa majina bandia ya ndugu, jamaa na marafiki.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Waziri Kairuki alisema mamlaka mbalimbali za dola zinashirikiana kwa karibu kufanikisha uhakiki huo, ambao utahusisha mlinganisho wa taarifa zilizotolewa na viongozi dhidi ya ukweli wa mali zao.

"Bajeti kwa ajili ya uhakiki huo ipo. Mwaka huu tutahakiki mali za viongozi 500 tukianza na viongozi 120 katika awamu ya kwanza.

Tutahakiki mali za viongozi wa aina zote. Watakaobainika wametoa taarifa za uongo, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria," alisema Kairuki.

Alizitaja baadhi ya taasisi zinazoshirikiana na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kufanikisha uhakiki huo ni Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na pia taarifa kutoka kwa wananchi.

Ipo pia Wizara ya Sheria na Katiba, chini ya waziri wake, Dk. Harrison Mwakyembe, lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa kila kiongozi anazingatia maadili ya uongozi wa umma.

Kairuki aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwafichua viongozi wanaomiliki mali kwa kificho, huku baadhi wakitumia majina ya ndugu na jamaa zao katika kuonyesha kuwa ndiyo wanaozimiliki.

“Pamoja na uhakiki huu kufanyika, tunaomba wananchi wajitokeze kwenda kukagua daftari lenye matamko ya mali na madeni ya viongozi wa umma ili kuweza kujua kiongozi yupi hasa amedanganya kuhusu mali zake,” alisema Kairuki na kuongeza:

"Wananchi ndiyo wanawajua zaidi… watatusaidia kujua kile alichokiandika katika tamko lake la kiapo, ndicho anachokimiliki au ameificha Sekreterieti."

UFAFANUZI WA KISHERIA

Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe, alipotafutwa na Nipashe jijini kuzungumzia suala hilo jana, alisema: "Kudanganya kiapo ni kosa kisheria na unaweza kushtakiwa."

Alisema mtumishi wa umma anayetoa taarifa za uongo kwenye kiapo chake, anakiuka sheria na anashtakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya Mwaka 1995.

Kwa kuzingatia maelekezo hayo, Nipashe ilifuatilia Sheria hiyo na kubaini kuwa kila kiongozi wa umma anabanwa ataje mali anazomiliki.

Kifungu 9(1) cha Sheria hiyo kinasema: "Kila kiongozi wa umma atatakiwa, isipokuwa tu kama Katiba au Sheria nyingine zilizoandikwa zitakapohitajika vinginevyo, kumpelekea Kamishna tamko la maandishi katika hati rasmi linaloorodhesha mali au rasilimali zake, au mume au watoto wenye umri usiozidi miaka 18 na ambao hawajaoa au kuolewa."

Aliyekuwa Kamishna wa Tume ya Maadili, Jaji Mstaafu Salome Kaganda, aliiambia Nipashe kwa simu ja kuwa utaratibu unaotumika endapo mtumishi wa Serikali akitoa taarifa za uongo kuhusu mali zake ni kumtaarifu kwa barua mhusika huyo ili azirekebishe.

Ikiwa mtumishi husika atashindwa kuzirekebisha, alisema Tume ya Maadili hufanya uchunguzi kwenye vyombo husika kama vile Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) na (TRA) ili kujua mali husika za mtumishi huyo.

Jaji Kaganda aliendelea kueleza kuwa endapo mtumishi husika akigundulika baada ya uchunguzi huo alitoa taarifa za uongo na kushindwa kuzirekebisha baada ya kupewa nafasi hiyo, atafikishwa katika Baraza la Maadili kwa kuwa ni kosa la jinai kutoa taarifa za uongo.

"Baraza la Maadili hufanya kazi na Jeshi la Polisi na Takukuru ambao huchukua hatua mara mtumishi anapokutwa na makosa," alisema Jaji Kaganda.

MALI KUFURU
Miongoni mwa mali zinazodaiwa kufichwa na viongozi wanaotumia nafasi zao kujilimbizia utajiri kufuru ni pamoja na nyumba za kifahari, magari ya bei mbaya, majengo ghali mijini yanayokodishwa kwa shughuli za biashara na ofisi, umiliki wa hisa kwenye kampuni mbalimbali, umiliki wa biashara kubwa kama za hoteli, vituo vya mafuta na magari makubwa ya mizigo, utitiri wa viwanja na mashamba makubwa.

“Kuna baadhi ya watu huonekana kuwa ni matajiri wakubwa mitaani lakini ukiwafuatilia utagundua kuwa wenye mali wanaohusishwa nazo siyo wao bali viongozi wasio waadilifu. Kadri nionavyo, itakuwa vigumu kwa watu wa aina hii kutobainika kupitia uhakiki huu wa mali halisi za viongozi,” mmoja wa maofisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (jina tunalihifadhi) aliiambia Nipashe jijini jana.

Alisema kuna 'vigogo' serikalini ambao wako kwenye idara na taasisi nyeti wanamiliki mali nyingi lakini wameziandikisha kwa majina ya ndugu na jamaa zao.

"Uongozi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma utaanza uhakiki mali zote muda wowote kuanzia sasa lakini kitengo cha uchunguzi kimetangulia na kimeshaanza kazi hiyo," alisema ofisa huyo.

Chanzo: Nipashe

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger