Moja ya nafasi inayosubiriwa kwa hamu kubwa ni nafasi ya katibu mkuu wa chama.
Kwa mtazamo wangu, miongoni mwa wafuatao wataukwaa ukatibu hiyo kesho:
1. Abdallah Bulembo: Ambaye kwa sasa ni mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi taifa ya chama cha mapinduzi ccm. Alifanya kazi kubwa katika uchaguzi wa 2015 uliomuweka madarakani mh. Rais Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa chama kwa sasa.
2. January Makamba: Kwa sasa ni waziri katika ofisi ya makamo wa rais anayeshughulikia masuala ya muungano na mazingira. Ni kada kindaki ndaki, kama ilivyo kwa Bulembo, pia naye alifanya juhudi kubwa sana katika kuhakikisha chama cha mapinduzi kinaibuka na ushindi wa kishindo. Alitajwa tajwa pia katika nafasi ya uwaziri mkuu mwanzoni mwa utawala wa Rais Magufuli.
3. Nape Moses Nnauye: Mwanasiasa kijana mkomavu ndani ya CCM. Kwa sasa anahudumu kama waziri wa michezo, habari, sanaa na wasanii katika serikali ya Rais JPM. Anakijua chama barabara, anafahamu mifumo ya chama kwa kuhudumu kama Katibu wa Nec itikadi na uenezi kwa muda mrefu.
Akishirikiana na Katibu wa sasa anayemaliza muda wake walikitoa chama kutoka ofisini na kukipeleka kwa wananchi. Mnakumbuka kipindi cha katibu mkama hali ilivyokuwa kabla ya Kinana na Nape.
Pamoja na majina hayo, pia kuna sura zinaweza kuingia kwa nafasi ya makamo mwenyekiti bara wa chama.
1. Asharozi Migiro
2. Abdullahman Kinana
3. Antony Diallo
Pia kati ya wafuatao mmoja wapo anaweza akawa makamo mwenyekiti Zanzibar.
1. Shamsi Vuai Nahodha
2. Pandu Amer Kificho
Mtazamo wangu tu.
By TAWA
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment