Aug 15, 2016

Aboud Jumbe Aacha Ujumbe Mzito, Ikiwemo Kukataa Kuzikwa Kifahari

Rais wa Pili wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi amefariki dunia mbele ya familia yake, akiwa ameacha ujumbe unaokataza mazishi yake kuhusisha taratibu zinazokiuka mafundisho ya dini ya Kiislamu.

Jumbe, ambaye alivuliwa nyadhifa zote serikalini na ndani ya CCM kutokana na kutofautiana na chama hicho katika suala la muundo wa Muungano, alishika nafasi ya urais mwaka 1972 baada ya muasisi wa Zanzibar, Abeid Amaan Karume kuuawa katika jaribio la mapinduzi.

Akizungumzia kifo hicho, mtoto wa Jumbe  Mustafa Jumbe amesema sababu ya kifo cha baba yake ni umri mkubwa ambao ni miaka 96.

Amesema kabla ya kuzikwa leo mwili, utaswaliwa katika msikiti wa Mwembeshauri na kuzikwa nyumbani kwake Migombani, Zanzibar.

“Marehemu ameacha wake wawili, watoto 14 na wajukuu zaidi ya 30,” amesema Mustafa.


Akataa kuzikwa kifahari

Mazishi ya kiongozi huyo aliyekaa madarakani kwa miaka 12 ikiwa ni muda mrefu kuliko marais wengine wa Zanzibar, yanaweza kutoshirikisha taratibu za kiserikali kutokana na wosia alioandika kabla ya kifo chake.

“Sitaki katika maziko yangu kutumbuizwa chochote kiendacho hata kidogo kinyume na mafundisho ya Islamu,” anaandika katika wosia huo.

“Sitaki beni (bendi), sitaki mizinga, sitaki maombolezo wala lolote jingine lenye hata chembe ya kufuru. Sitaki hivyo nikiwa hai, nitakapoondoka katika dunia. Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi wangu, duniani na akhera.”

Kwa kawaida kiongozi wa kada yake anapofariki, hupigiwa mizingi 21 na kusubiri taratibu za kiserikali ambazo wakati mwingine huchukua muda kukamilika tofauti na sheria za dini hiyo.



Magufuli atuma salamu

Kutokana na kifo hicho, Rais John Pombe Magufuli na viongozi wengine mbalimbali wa Serikali wametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Jumbe, wakielezea kusikitishwa na msiba huo.

Rais Magufuli ametuma salamu hizo kwa Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein na kusema kuwa Taifa limempoteza mtu muhimu ambaye alijitoa kupigania uhuru, umoja, haki na maendeleo ya wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika kipindi kigumu ambacho Taifa lilikipitia.

“Nimeshtushwa sana na kifo cha mzee wetu,  Aboud Jumbe. Kwa hakika Tanzania imepoteza mtu muhimu ambaye katika kipindi cha uongozi wake alitoa mchango mkubwa wa kuipigania na kuijenga Tanzania tunayoiona leo,” amesema  Rais Magufuli katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa.

“Kupitia kwako Dk Shein, napenda kuipa pole familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki wote, wananchi wa Zanzibar na Watanzania wote kwa ujumla kwa kufikwa na msiba huu mkubwa.”

 Mbowe amkumbuka

Akizungumzia kifo hicho, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitoa pole kwa niaba ya chama hicho kikuu cha upinzani kwa familia na Serikali ya Tanzania na Zanzibar.

Mbowe alisema serikali hizo mbili zilimtenga kwa muda mrefu kiongozi huyo kwa kile alichoeleza kuwa ni kukinzana na msimamo wa chama chake wakati wa utawala wa Mwalimu Julius Nyerere.

Alisema msimamo wa Jumbe kuhusu Zanzibar na wa chama chake ni mfano wa kuigwa.



CCM washtushwa

Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka alisema wameshtushwa na kifo cha Jumbe.

Alisema kiongozi huyo atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa wakati uongozi wake hasa wakati chama cha Afro-Shiraz (ASP) kilipoungana na Tanganyika African Nation Union (Tanu) na kuunda CCM mwaka 1977.


CUF waomboleza

Pia, CUF imetoa salamu za rambirambi kwa Wazanzibari na Watanzania wote kutokana na kifo hicho.

Mkurugenzi wa habari, uenezi na mahusiano wa chama hicho, Salim Bimany alisema wamepokea msiba huo kwa masikitiko makubwa na watamkumbuka kama kiongozi wa mwanzo baada ya Mapinduzi ya 1964 aliyefungua milango ya demokrasia kwa kuanzisha chombo cha kuwasemea wananchi wa Zanzibar ambacho ni Baraza la Wawakilishi lililoanzishwa 1980.

“Alhaj Jumbe ndiye aliyetandika misingi ya kidemokrasia Zanzibar na kuanzisha utawala wa sheria na katiba.  Yeye ndiye aliyeurejesha mhimili wa mahakama uliopotea baada ya Mapinduzi kwa kuwa Zanzibar ilikuwa ikitawaliwa kwa amri za kijeshi,” alisema Bimany.

“Alipunguza makali ya mkono wa chuma, madaraka ya kiimla na kuwaondoshea hofu wananchi. Kusema kweli alijitahidi kwa mujibu wa uwezo wake na mazingira yaliyokuwapo kuhakikisha Zanzibar inapata hadhi na mamlaka yake ya kinchi. Ni mtu aliyekisimamia anachokiamini,” alisema mkurugenzi huyo wa habari wa CUF.

 Sheikh asimulia

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu, Sheikh Mohamed Issa wa Dar es Salaam alisema anamkumbuka Alhaj Jumbe kwa kuwa mkweli na muwazi pamoja na mitihani yote aliyoipata.

“Kama miaka sita nyuma nilik



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger