Sep 19, 2016

ACT-Wazalendo Wambipu Magufuli..Watangaza kufanya kongamano la kidemokrasia Septemba, 24


Chama cha ACT – Wazalendo kimetangaza azma yake ya kufanya mkutano mkuu wa kidemokrasia Jumamosi ijayo licha ya kuwapo kwa amri ya Polisi iliyokataza kufanyika kwa mikutano yote ya kisiasa nchini. 

Jeshi la Polisi lilipiga marufuku maandamano na mikutano yote ya hadhara tangu Juni 7 hadi pale hali ya usalama itakapotengemaa. 

Jeshi hilo lilisema limefikia hatua hiyo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa vyama vya siasa vikitaka kufanya mikutano na maandamano kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kutotii sheria za nchi.

Lakini jana, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT – Wazalendo, Ado Shaibu alisema wamepanga kufanya mkutano huo kwa sababu Katiba inawaruhusu.

“ACT kimekusudia kuitisha mkutano mkuu wa kidemokrasia, hii ni haki yetu kikatiba na hata kwa dunia nzima si ajabu kwa kuwa vyama vya siasa hufanya hivyo. Kongamano hili litawaleta pamoja wanachama, wadau na wafadhili wa ACT ambao watajadili hali ya maendeleo ya nchi,” alisema na kuongeza.

“Hatutaji mahali na ukumbi tutakaoufanyia kwa sasa, wakati ukifika tutawajulisha.Na hatutaomba kibali kwa kuwa katiba haisemi vyama vya siasa viombe  kibali vinapotaka kufanya mikutano ya ndani.”

Shaibu alisema kuwa endapo serikali itazuia kufanyika kongamano hilo watachukua hatua za kisheria kupinga maamuzi hayo kwa madai kuwa katiba ya nchi na ya vyama vya siasa inarushusu kufanyika.

“Serikali ilituzia kufanya mikutano na vikao vya ndani, tulikaa kimya awali tukiamini kuwa tutaishawishi kwa hoja na itajirekebisa lakini haikufanya hivyo.Tunaamini serikali itarudi nyuma na kuamini haina mamlaka ya kuzuia mikutano na vikao vya ndani kwa sababu kuizuia inamaana unafuta shughuli za siasa na sisi tutakuwa wa mwisho kukubali vyama kufutwa ,” alisema.

Alisema ACT haitokuwa nyuma kuiunga mkono serikali inapofanya vyema na kwamba endapo chama hicho kitakosoa utendaji kazi wake, serikali isikichukie kwa kuwa kinatekeleza wajibu wajibu wake.

Kwa upande mwingine, Shaibu alisema Kamati Kuu ya Uongozi wa Chama cha ACT imefanya baadhi ya marekebisho ya muundo wa uendeshaji kwa kuteua baadhi ya makatibu wa kamati za chama hicho.

“Kikao cha tatu cha kamati kuu kilichoketi Septemba 5,2016 kilifanya teuzi mbalimbali za makatibu, sambamba na kugawa baadhi ya kamati ikiwemo iliyokuwa kamati ya Ulinzi, Usalama na Uadilifu ambapo kwa sasa imegawanyika na kuwa kamati ya Usalama na Ulinzi na mpya ni Kamati ya Uadilifu, ” alisema.

Aliwataja makatibu wapya wa kamati walioteuliwa akiwemo aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Chama cha Wananchi CUF (JUVICUF) Mohamed Babu ambaye kwa sasa ni Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Ally Kifu ameteuliwa kuwa Katibu wa kamati ya Fedha na Miradi ya Kujitegemea. Katibu mwingine aliyeteuliwa ni Sabrah Mohamed ambaye ameshikilia Kitengo cha Kushughulikia Maendeleo ya Zanzibar.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger