Sep 13, 2016

Kaka Yangu Julius Mtatiro, Usifuate Njia ya Waliopotea


Linaandika Gazeti la Mwananchi; ''BUNDI WA TIMUA TIMUA ATUA CUF NYAMAGANA'' katika habari kuna taarifa kuwa Viongozi waandamizi watano (5) wa CUF wilayani Nyamagana wamefukuzwa. Viongozi hao akiwemo Mwenyekiti wa Wilaya hiyo Ndg Salum Mkumbukwa, aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo Ndg Faida Potea, Mkurugenzi wa Mipango na Chaguzi Mohamed Makongoro, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Hamza Shido, Omary Abubakar Mkurugenzi wa Utawala na Nazar Nyampangula Mkurugenzi wa Siasa, taarifa hiyo ikaendelea kudai kuwa Viongozi wengine 2 wamewekwa chini ya uangalizi maalum ambao ni wakurugenzi wa Idara ya Fedha na Ulinzi. 

Sababu kubwa iliyotolewa ni kuwa Viongozi hao hawakuwasilisha taarifa za mpango kazi wa ofisi yao. Ukiitazama sababu hii "KUTOWASILISHA TAARIFA ZA MPANGO KAZI WA OFISI" na kuilinganisha na adhabu ya kufukuzwa, utajiuliza maswali ambayo yanaweza kusababisha mtikisiko mkubwa wa ubongo, ni jambo haliingii akilini.

Haiitaji kuwa msomi wa chuo kikuu kujua kuwa sababu sio hiyo, ila kwa kuwa sababu yenyewe haiwezi kuwekwa hadharani, inatafutwa sababu nyingine "cover up" ya kujustify maamuzi ya kufukuzana.

Hili ni moja ya tatizo kubwa ndani ya vyama vya siasa vya upinzani, tatizo hili limeshakuwa donda ndugu ambalo limeshakuwa la kudumu kwa upinzani. Vyama hivi ambavyo vinadai na kupiga kelele ya udikteta na kuminywa kwa demokrasia nchini, ni kama vile vinatazama kibanzi kwa jicho la jirani ikiwa kwao kuna Boriti. 

Kwa tafsiri ya shule na iliyo kikatiba, Chama cha Siasa** ni muungano wa watu (wanachama) wenye itikadi fulani waliopania kuishika na kuendesha serikali. Chama ni wanachama, sera na itikadi. kwa tafsiri hii vyama vingi vya upinzani Tanzania havina qualification ya kuwa vyama vya siasa, maana vyama hivyo vina wamiliki (ambao sio wanachama) ambao wakiamua iwe hivi inakuwa hivyo na wakiamua kufukuza yeyote kwa maslahi yao wanafanya hivyo. Vyama havina sera wala itikadi inayoeleweka.

Ni vigumu leo kutofautisha umiliki wa Mbowe kwa Tanzania Daima ama Protea hotel na Umiliki wake wa CHADEMA, namna anavyooperate, anavyotoa amri na kusimamia execution ya mikakati yake ni kama vile CHADEMA ni mali yake kamili ambayo anao mpango wa kuirithisha kwa wanawe.

Spika wa Bunge Tukufu la Jamhuri alijaribu kuwasihi na kuwashauri wapinzani juu ya tabia hii ya hovyo ya kufukuzana kila asubuhi. Lakini ni kama wana masikio na hawasikii na wana macho na hawaoni.

Kinachosikitisha ni pale ambapo hata Viongozi vijana ambao tulidhani wakati fulani kuwa tunaweza kushirikiana nao kuijenga TANZANIA NJEMA, nao wamekuwa wafuasi wakubwa wa hulka na mwendo huu wa upotevu. Mtatiro, kaka yangu utafukuza wangapi..? Maana watu si mawe kuwa utayageuza unavyotaka, kila asubuhi atatokea kwa kuhoji na kuuliza kwanini unigeuze, utafukuza wote..??? ili ubaki na nani..? 

Imezaliwa ACT ikiwa ni alama ya kudumu ya udikteta wa MBOWE, Mtatiro unataka kuzalisha ACT nyingine..? Wakati mwingine tujifunze kupevuka kiakili, haya mambo yana mwisho. Waswahili wanasema hata mwisho una mwisho wake.....hautabaki MWENYEKITI wa MPITO milele...itendee haki nafasi yako, vijana wenzako tujivunie kuwa umeipitisha CUF katika wakati mgumu na ukaiacha salama. KUFUKUZANA hakutokuacha wewe salama wala CUF haitabaki salama.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger