Sep 12, 2016

Tume Ya Mufti Yawaita Wanaojua Wezi Bakwata

TUME iliyoundwa na Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakari Zuberi kuchunguza mali za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), imeomba watu wenye taarifu juu ya ubadhirifu wa mali za taasisi hiyo wawasiliane nao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo, Sheikh Issa Othman Issa aliomba pia ushirikiano wa watu wenye taarifa juu ya mali za baraza hilo.

Sheikh Issa aliahidi kuwa tume yake itawalinda wale wote watakaowapa taarifa zozote zitakazosaidia katika uchunguzi wao.

“Tunaendelea kuwaomba wale wenye taarifa za mali za Waislamu ambazo ziko chini ya usimamizi wa Bakwata wawasiliane na tume ikiwamo kukabidhi nyaraka zote walizonazo, hata wenye ushahidi wowote wa ubadhirifu wa mali wazilete tunaahidi kwa dhati tutazifanyia kazi na kuwalinda watoa taarifa, tume hii ni huru ina ruhusa ya kuendesha kazi zake bila kuingiliwa na mtu ama chombo chochote,” alisema Sheikh Issa.

Alisema katika kufanikisha kazi hiyo waliyopewa, tume hiyo inafanya kazi na jopo la wataalamu na vyombo mbalimbali vilivyobobea katika masuala hayo.

Sheikh Issa alisema wamepewa hadidu za rejea saba ikiwamo kuchunguza misamaha ya kodi iliyotolewa kwa baraza na taasisi zake.

Kuundwa kwa tume hiyo ni matokeo ya ushauri uliotolewa na Rais John Magufuli, Julai mwaka huu alipokuwa akihutubia Baraza la Eid ambapo pia aliahidi kuzirejesha mali zilizoporwa za waumini wa dini hiyo.

Sheikh Issa alisema kuwa wamepewa miezi mitatu kukamilisha uchunguzi huo.

Alitaja mambo watakayochunguza kuwa ni pamoja na misamaha ya kodi iliyoombwa na Bakwata nchi nzima, mikataba yote ya uuzaji wa viwanja na mali mbalimbali za baraza na taasisi zake pamoja na uhalali wa umiliki wake.

Nyingine ni kutafuta mikataba yote ambayo baraza na taasisi zake zimeingia na wawekezaji na kuona mikataba hiyo kama ina maslahi na baraza au laa, na kuchunguza mikataba yote ambayo taasisi zake nchi nzima zimeingia na wapangaji wake katika maeneo mbalimbali yanayomilikiwa na baraza hilo.

Nyingine ni kuchunguza mali zote za baraza na kuona hali ya usajili wa mali hizo na kuchunguza mapato na matumizi ya baraza hilo na taasisi zake nchi nzima.

Sheikh Issa alisema baada ya uchunguzi huo kukamilika ndani ya siku hizo 90 watakabidhi ripoti hiyo kwa Mufti kwa ajili ya hatua nyingine zaidi.

Wakati huo huo, swala ya Eid El-Hajj inatarajiwa kuswaliwa leo makao makuu ya Bakwata, yaliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari jana na Katibu wa Baraza hilo, Salim Abeid, swala hiyo itaambatana na Baraza la EID na kufuatiwa na uzinduzi wa Chuo cha Kiislam.

Abeid alisema swala hiyo itafanyika saa moja na nusu asubuhi na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger