Nov 3, 2016

Ufisadi Wagubika Shirika la Posta.....Bodi Yabaini Mikataba Mibofu, Rushwa na Upendeleo katika Ajira

Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC) imebaini madudu lukuki, ikiwamo mikataba mibovu, idadi kubwa ya wafanyakazi wenye elimu ya chini, rushwa na kuajiri kwa upendeleo.

Akizungumza na wanahabari jana, mwenyekiti wa bodi hiyo, Dk Haruni Ramadhani alisema shirika linakabiliwa na “maradhi” mengi ambayo kama hayatashughulikiwa ipasavyo yanaweza kusababisha malengo kutotekelezwa kwa ufanisi.

Kutokana na madudu hayo, bodi imeipa miezi sita menejimenti ya TPC kurekebisha kasoro hizo na kinyume na hapo, hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

“Tumebaini Shirika la Posta lina uwezo na fursa kubwa kama tutaitumia vizuri kuchangia Pato la Taifa. Ni shirika ambalo limesambaza huduma zake toka ngazi ya Taifa, kata na vijiji. Posta ina mizizi mingi mikubwa na imara,” alisema.

“Kinachokosekana ni utashi na kujituma, ubunifu na utendaji kazi kwa weledi na umakini. Lazima sasa tubadilike, tuache kufanya kazi kwa mazoea, uzembe, ubinafsi, ufisadi, wizi na rushwa. Vitu hivi lazima tuambizane ukweli bila kuoneana aibu. Havina nafasi tena Posta,” alisema.

Mikataba Mibovu
Dk Ramadhani alisema wakati bodi hiyo ikiendelea na uchunguzi, imebainika shirika hilo liliingia mikataba mibovu ukiwamo ule wa kati ya TPC na kampuni ya Wande Printing and Packaging.

Katika mkataba huu, bodi ilibaini kuwa Wande Printing and Packaging walipangisha jengo la ghorofa tatu (mali ya shirika) kwa Sh1.8 milioni kwa mwezi, kwa muda wa miaka mitatu ambayo ni sawa na Sh64.8 milioni.

Alisema baadaye, mwekezaji alifanya ukarabati wa jengo kwa Sh398 milioni, hivyo ili kufidia fedha hizo, mkataba huo ulieleza Wande Printing and Packaging itakaa kwenye jengo hilo bila kulipa kwa miaka 20 ili kufidia fedha zake.

Mwenyekiti huyo alisema mkataba mwingine ni kati ya TPC na kampuni ya Universal G & G ambao ulihusisha upangishaji wa jengo lililopo kitalu namba 416 Block G, Ubungo. Alisema katika mkataba huo Universal G & G na TPC waliingia mkataba wa kudumu na TPC ina hisa asilimia 25 na Universal asilimia 75.

Kaimu Posta Masta wa TPC, Fortunatus Kapinga alisema waliingia kimakosa mkataba wa jengo la Posta lililo karibu na Mawasiliano Tower, na sasa wapo kwenye utaratibu wa kuzungumza na mwanasheria wa kampuni.

Pamoja na mikataba mibovu, Dk Ramadhani alisema baadhi ya watumishi wa shirika hilo wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya rushwa kwa kufanya malipo hewa kwa wastaafu wa Shirika la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii wakitumia mfumo wa Post Giro.

Post Giro ni mfumo wa kizamani wa malipo kutoka benki moja kwenda benki nyingine na mlipaji ndiye huidhinisha malipo yote.

Mwenyekiti huyo aliyataja madudu mengine waliyobaini ndani ya shirika hilo kuwa ni kuwepo na tabia ya kupeana ajira kwa upendeleo, kupandishwa vyeo kwa rushwa, fedha au rushwa ya ngono.

“Kwa mfano vijana walioteuliwa na ofisi ya General Manager, Corperate Resource Management baadhi yao wana dalili za kujihusisha na rushwa. Mfano watumishi waliokuwa na vyeti feki wengi wao walisaidiwa kuviondoa katika majalada yao,” alisema.

Pamoja na madudu hayo mwenyekiti huyo alisema wamebaini ufanisi unadorora kwa kuwa zaidi ya wafanyakazi 120 wana elimu ya darasa la saba na zaidi ya 1,000 wameishia kidato cha nne.

“Wale wote wenye tabia ya wizi, umangimeza, rushwa, ubadhilifu na ufisadi hawana nafasi,” alisema.

Dk Ramadhani alisema shirika hilo linasuasua kutokana na wingi wa madeni na hadi Juni, 2016 lilikuwa linadaiwa Sh20.5 bilioni. Kati ya fedha hizo, Sh16 bilioni ni makato ya wafanyakazi yanayotakiwa kwenda Mamlaka ya Mapato (TRA).

Pia, alisema TPC inaidai Serikali Sh5.5 bilioni, taasisi za umma Sh1.9 bilioni, watu binafsi Sh1.8 bilioni na hivyo kulitaka kuongeza juhudi katika kukusanya madeni.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger