Nov 3, 2016

Wapakistani Wahukumiwa Miaka Minne Jela Kwa Kuingiza Vifaa vya Mawasiliano Bila Lesen

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu raia watatu wa Pakistan, kifungo cha miaka minne jela au kulipa faini ya Sh milioni 125 baada ya kupatikana na hatia ya kuingilia mtandao wa mawasiliano na kuisababishia serikali hasara ya Sh milioni 145.

Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage, alitoa hukumu hiyo baada ya washtakiwa, Hafees Irfan, Mirza Irfan Baig na Mirza Rizwani Baig, kukiri makosa yao.

Akitoa adhabu hiyo, Hakimu Mwijage alisema, washtakiwa wamepatikana na hatia ya makosa manne na katika kila kosa watalipa faini ya Sh milioni tano au kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela, ambayo ni sawa na faini ya Sh milioni 20 au kifungo cha miaka minne jela.

Aidha, alisema kwa sababu mashtaka yanahusisha kuisababishia hasara Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), kila mshtakiwa anatakiwa kulipa faini ya Sh milioni 35, pia washtakiwa wakimaliza kutumikia vifungo vyao, warud ishwe nchini kwao na vifaa walivyokutwa navyo vitakuwa mali ya serikali.

Awali, kabla ya hukumu hiyo, Wakili wa Serikali Esther Martin aliwasomea washtakiwa hao maelezo ya awali na kudai kuwa katika tarehe tofauti, Dar es Salaam, washtakiwa walikutwa na vifaa vya kuunganishia mawasiliano ya kimataifa bila kuwa na kibali cha TCRA.

Alidai, washtakiwa walitoka Pakistan na kwenda maeneo mbalimbali ikiwemo Arab Emirates, Malaysia, Msumbiji kwa ajili ya kutumia vifaa hivyo, pia waliingia nchini katika tarehe tofauti na kufikia kwenye chumba namba 905 katika Hoteli ya Butterfly iliyopo Kariakoo, Dar es Salaam.

Inadaiwa wakiwa kwenye chumba hicho, waliunganisha mawasiliano kwa kutumia vifaa vya kimataifa bila kuwa na kibali cha TCRA, lakini wakati wakiendelea na kazi zao ilibainika kuwa, kuna watu katika maeneo hayo wanatoa huduma ya mawasiliano, kinyume cha sheria.

Aliendelea kudai kuwa, Oktoba 5, mwaka jana, maofisa wa Polisi wakiambatana na TCRA walifika maeneo hayo na kufanya upelelezi, kisha wakawakamata washtakiwa hao katika hoteli wakiwa na vifaa mbalimbali vya mawasiliano, ambavyo ni kadi za simu 273, CPU 18, Laptop saba, Moderm ya Huawei na vocha zilizokwishatumika.

Washtakiwa walifikishwa kituo cha Polisi Kijitonyama na baada ya kufanya upelelezi, ilibainika kuwa wameisababishia serikali na TCRA hasara ya Sh milioni 140.

Baada ya kusomewa maelezo yao, washtakiwa walikiri makosa. Wakili Esther aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa washtakiwa ili iwe fundisho kwa wengine na makosa hayo, yasiwe yanajirudia rudia, adhabu itolewe kwa kuzingatia hasara walioisababisha washtakiwa, pia alidai makosa hayo yanahatarisha usalama wa taifa.

Hata hivyo, Wakili wa utetezi, Shadrack Ishengoma aliiomba mahakama hiyo kuwapunguzia adhabu hiyo washtakiwa kwa sababu wamekiri makosa yao, pia wanategemewa na familia zao, na kuongeza kuwa washtakiwa wameshakaa rumande kwa miezi 13 yaani zaidi ya mwaka mmoja.

Hakimu Mwijage alisema ametoa adhabu hiyo kwa kuzingatia hoja za pande zote mbili na washtakiwa walilipa faini na kuachiwa.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger