Mara zote tunawasikia wafuasi wa chadema na viongozi wao wakijigamba kuwa "Tutawapiga Mahakamani". Kwamba, wao wana mawakili bora sana hapa Tanzania na kwa hiyo kiongozi au mfuasi yeyote wa chadema anaweza kusema ama kufanya lolote kwani kisheria Serikali haina nguvu. Hizi ni dharau za hali ya juu sana ambazo kwa hakika zinapaswa kukomeshwa.
Lema yupo Mahabusu sasa. Haijulikani lini atatoka kwa vile uzito wa mashtaka yanayomkabili ni mkubwa sana. Kesi zinazomkabili zinachukuliwa kwa uzito mkubwa sana kwa sababu ametoa kauli ambazo si tu hazikupaswa kutolewa na mtu kama yeye bali hata na mtu mwingine yeyote.
Kumzulia kifo Mkuu wa nchi ni kosa la uhaini ambalo kwa nchi nyingine huchukuliwa kwa uzito mkubwa sana na adhabu yake ni kifo. Sina hakika kwa sheria za hapa kwetu. Hii ni kwa sababu unaposema Mkuu wa nchi atakufa kabla ya muda fulani maana yake ni kwamba wewe mwenyewe unaingilia Malmala ya Mungu ambaye ametanabaisha kwenye vitabu vyake kuwa hakuna ajuaye siku wala saa ya mtu kuondoka duniani isipokuwa Yeye.
Rais kama Mkuu wa nchi anao maadui wengi hasa kwa huyu ambaye kila uchwao anatumbua. Kupitia kauli ya Lema maadui wa Rais wanaweza kutembea na maneno yake na wakafanikisha mauaji ya Rais ili watu waamini kuwa alichoongea Lema kimetimia.
Pia ikiwa Lema ataachwa huru, anaweza kushiriki kwenye mipango ya kumdhuru Rais ili tu kutimiza maono yake. Lema si wa kispot kispot. Ameshiriki matukio mengi makubwa ambayo kama yakiwekwa hapa hadharani hakika hakuna atakayemuamini Lema. Msifikiri ni masihara pale watu wanaposema kuwa kazi yake ya mwanzo kabla hajawa Mbunge ni ya kutisha sana. Si masihara hata kidogo.
Mkumbuke kuwa kwenye kurasa zao za Facebook wafuasi wengi wa CHADEMA wanatamani Rais afe hata leo kitu ambacho kwa hakika si kizuri.
Yanayomkuta Lema yawe fundisho kwa wengine. Kipindi hiki tu cha Lema kuwa Mahabusu naona nidhamu imeanza kurejea. Zitto Kabwe katelekeza Akaunti yake ya Twitter tangu Oktoba 21. Ni akaunti hiyo ndiyo aliyokuwa anatumia kuandika mabaya dhidi ya Rais.
Julius Mtatiro naye kaamua kurejea kazi yake ya awali ya uchambuzi. Biashara ya kumshambulia Rais hailipi.
Tundu Lissi naye kaamua kujirekebisha. Aliahidi kupambana na Rais kiangazi na masika ila kwa yanayomkuta Lema hakika hathubutu tena. Kikubwa zaidi ni pale Lissu alipojiengua kumtetea Lema baada ya kuona uzito wa kesi yenyewe.
Naamini kuwa wanasiasa wataendelea kujifunza kupitia sakata hilo la Lema.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment